Habari za Punde

Chama cha Mapinduzi (CCM) Chasisitiza Amani Nchini

Katibu wa kamati maalum ya NEC ,Idara ya itikadi na uwenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao akiwaonyesha Waandishi wa Habari ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2020 ambayo inasisistiza amani, huko Afisi kuu za CCM Kisiwandui Zanzibar.
Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali wakimsikiliza Katibu wa kamati maalum ya NEC ,Idara ya itikadi na uwenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao (hayuko pichani)wakati akitoa tamko kuhusu vitendo vya uvunjaji wa Amani hasa kipindi hichi cha uchaguzi huko Afisi kuu za CCM Kisiwandui Zanzibar.
 

Na Mwashungi Tahir    Maelezo .

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wametakiwa kuwa watulivu  kutokana na tukio lililotokea huko kisiwani Pemba la kupigwa mapanga watu watatu wakiwa katika sehemu ya kufanyia Ibada.

Akizungumza na waandishi wa habari  Katibu wa Kamati maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Catherine Peter Nao kuhusiana na  tukio hilo  huko katika ukumbi wa Afisi ya Kiswandui na kulaani kwani ni tendo la kinyama na kusikitisha jamii.

Amesema nchi bado ina amani na kuwataka wanachama kuwa watulivu,  kuondosha hofu kwani  Jeshi la Polisi linafanya kazi yake na wahusika wanafuatiliwa ili  hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Hata hivyo amesema lengo la kufanya vitendo hivyo ni kuwatia woga wanachama wa CCM huko Pemba ili ikifika siku ya kupiga kura waogope kufika vituoni na kuchagua viongozi wanaowataka.

“Kufanya hivyo ni kutaka kuwatia hofu ili muogope kwenda kupiga kura lakini ondosheni hofu na ikifika siku jitokezeni kwa wingi kwenye vituo vya kupiga kura kwani vyombo vya ulinzi vitaimarishwa zaidi”,alisema Catherine.

 Aliwaomba wananchi wawe watulivu na Chama cha Mapinduzi kipo  pamoja na waliofikwa  na kadhiya hiyo,na kuwataka familia iwe na subra 

Pia amesema CCM sio chama cha kulipiza kisasi mambo ambayo hayafai katika jamii kwani chama hicho hufuata miongozo iliopo ndani ya ilani na kinaongoza  vizuri na  kukubalika na jamii kuongoza dola.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.