Habari za Punde

ZEC Yawataka Taasisi za Asasi Kiraia Kutoa Elimu ya Mpiga Kura Kuzingatia Jinsia.

 Na JaalaMakame Haji- ZEC

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imezitaka Asasi za kiraia ambazo zimepewa vibali vya kutoa elimu ya wapiga kura kuzingatia zaidi matakwa ya sera ya jinsi na ushirikishwaji wa makundi ya kijamii ya mwaka 2015 iliyoanzishwa na tume kwa lengo la kuyashirikisha kikamilifu makundi hayo katika masuala ya uchaguzi

Akifungua mkutano ambao umeshirikisha Asasi za kiraia, makundi ya vijana na wanawake huko katika ukumbi wa kituo cha  waandishi, waangalizi na matukeo ya uchaguzi maruhubi, Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe. Jaji Mkuu (mst) Hamid Mahmoud Hamid alisema Tume imewaamini na kuwapa vibali vya kutoa elimu kwa jamii ili waweze kushiriki kikamilifu katika masuala ya Uchaguzi.

Akiwasilisha mada kuhusu matayarisho ya uchaguzi mkuu 2020 Mkurugenzi wa uchaguzi Thabit Idarous Faina alieleza kuwa, bajeti na mpango kazi wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 uliandaliwa na kuwasilishwa Serikalini ambapo Serikali imeipatia Tume mahitaji yote ya bajeti iliyowasilishwa kukamilisha majukumu yake.

hadi tunavyozungumza katika mkutano huu uagiziaji wa vifaa na huduma za Uchaguzi zimekamilika. Karatasi za kura zinaendelea na hatua ya uchapishaji ambao unatarajiwa kukamilika wiki mbili kabla ya siku ya uchaguzi ili ziweze kusambazwa kwa wakati” alisema.

Akizungumza kuhusu kura ya mapema Mkurugenzi Faina alisema tarehe 27 Oktoba, 2020 ZEC itaendesha kura ya Mapema ambayo itahusisha watendaji wa Uchaguzi na walinzi wanaohusika na ulinzi na usalama siku ya Uchaguzi ili watu hao waweze kupiga kura ya mapema.

Hata hivyo, Ndugu Faina alifafanua kuwa, Wapiga Kura wa Kura ya mapema wakiwemo wale wanaohusika na ulinzi na usalama siku ya Uchaguzi ni lazima wawe wameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura

Akizungumza kwa niaba ya mrajis wa asasi za kiraia Mwanabaraka Saleh Sheha amezitaka asasi kufuatu amaelekezo ya tume ambayo ni muhimu katika katanua wigo wa kuelimisha umma katika hatua zote za uchaguzi.

Nao washiriki wa mkutano wamewataka wananchi kutafakari na kufanya maamuzi sahihi katika kuchagua viongozi siku ya kupiga kura.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.