Hayo
yalisemwa na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Khamis Juma Mwalim wakati akifungua
mkutano wa siku mbili wa wasaidizi wa sheria wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za
Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa Hotel ya Zanzibar Beach Resort nje
kidogo ya mji wa Zanzibar.
Waziri
Khamis alisema Serikali mbili hizo zinawaunga mkono wasaidizi wa kisheria
kutokana na njia muhimu ya kufikia maendeleo endelevu ya dunia (SDG).
Alisema
ushirikiano wa wasaidizi wa kisheria katika nchi za
SADC utaweza kuwasaidia wananchi wenye uwezo mdogo kupata haki yao
ya msingi kutokana na matatizo wanayokumbana nayo.
“Serikali
zetu mbili za SMT na SMZ imejidhatii kuhakikisha inawaunga mkono kikamilifu
wasaidizi wa kisheria katika kutatua matatizo na kuwaletea mataendeleo wananchi
wanyonge,”alisema.
Waziri
Khamis alisema Zanzibar imefanikiwa kupitisha Sheria ya Msaada wa
kisheria mwaka 2018 kutokana na umuhimu uliokuwepo wa kulizungumzia
hilo kutokana na baadhi ya wananchi hawajui umuhimu wa kuwepo kwa wasaidizi
hao.
Hivyo
aliwaomba wananchi wa Zanzibar kuitumia Idara ya Msaada wa Kisheria kwani ipo
kwa ajili yao na imejipangia mikakati ya kuwafikia wananchi wote kwa kuweka
ofisi kwenye Wilaya zote ili kuwafikia wananchi wake.
Waziri
Khamis amewashukuru waandaji wa mkutano huo pamoja na waliofanikisha kufanyika
kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo endelevu ya nchi na kwamba huduma za
kisheria zinahitaka kumfikia kila raia.
Nae Katibu
Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Profesa
Sifuni Mchome alisema mwaka 2017 SMT imepitisha sheria ya kuwatambua na kwa
sasa wamesambaa nchi nzima .
Alisema
tayari wasaidizi wa kisheria Tanzania Bara wanatambulika kisheria na wamekua
wakitoa msaada mkubwa kwa wananchi wenye mahitaji hayo katika maeneo mbali
mbali.
“Wasaidizi
wa kisheria Tanzania Bara wanafanya kazi vizuri na wanatambuliwa na Serikali
lakini changamoto kubwa zinazowakabili ni ukosefu wa fedha pamoja na uelewa
mdogo miongoni mwa wananchi,”alifafanua.
Akizungumza
kabla ya ufunguzi wa mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Msaada wa Kisheria
Hanifa Ramadhan Said alisema mkutano huo umefanyika wakati muafaka kwa
kubadilishana uzoefu na kuendeleza mbele huduma za kisheria kwa wananchi
hususan maskini na wenye mahitaji maalum vijijini.
Mkutano
huo ulitarajiwa kufanyika mwezi wa sita mwaka huu, kutokana na kuzuka kwa
maradhi ya homa kali ya mapafu inayotokana na virusi vya corona na
umefanyika leo ambapo baadhi ya wanachama wa shiriki wa jumuiya hiyo ambao
hawajaweza kufika wanahudhuria mkutano huo kwa njia ya mtandao wa kijamii wa
Zoom.
No comments:
Post a Comment