Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein Amefungua Kongamano la Amani na Kuiombea Nchi Dua ya Amani leo. 7/10/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Alhajj Balozi Seif Ali Iddi alipowasili katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) kuhudhuria  Kongamano la Amani lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar, kuiombea Dua Nchi kuendelea na Amani baada ya Uchaguzi lililofanyika leo 7-10-2020. Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj.Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi, alipowasili katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) kuhudhuria hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Amani  kuiombea Nchi Dua lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar.
Viongozi wa Dini Zanzibaer wakiwa wamesimama wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) kwa ajili ya hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Amani kuiombea Nchi Dua. lililofanyika leo Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein akiwa na Viongozi wa meza kuu wakiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, kabla ya kuaza kwa Kongamano la Amani kuiombea Dua Nchi kuendelea na Amani lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar. Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Ungyuja leo.
Wagombea Urais wa Zanzibar  wa kwanza Mgombea Urais kupitia Chama cha ADC Mhe. Hamad Rashid Mohammed akiwa na Mgombea Mwezake wa Urais kupitia Chama cha ADA-TADEA Mhe Juma Ali Khatib, wakiitikia dua wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Amani lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar. lililofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusiniu Unguja leo.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar Sheikh Fadshil Soraga, akizungumza na kutowa taarifa fupi ya Kongamano la Amani Zanzibar kabla ya kuaza kwake katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) leo asubuhi. 
Waumini wa Dini Zanzibar na Wananchi wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa Kongamani la Kitaifa kuitakia Amani Zanzibar kwa Dua iliofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) Wilaya ya Kati Unguja leo.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha ADC Mhe Hamad Rashid Mohame akizungumza wakati wa hafla ya Kongamano la Dua kuiombea Nchi Amani lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar lililofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein. Tunguu (SUZA)  na kuwataka Wananchi kuitunza Amani hasa kiupindi hichi cha Uchaguzi na baada ya uchaguzi kudumisha Amani Nchini.
Mgombea Urais wa Zanzibar kuypitia Chama Cha ADA-TADEA  Mhe. Juma Ali Khatib akisisitiza jambo wakati akuzungumza katika hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Amani kuiombea Nchi lililoandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar, katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) Wilaya ya Kati Unguja leo.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akuzungumza katika mkutano wa Kongamano la Amani kuitakia Nchi Amani kwa Dua iliofanyika katika ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) na kuwataka Wananchi wa Zanzibar kuilinda Amani ya Nchi katika kipindi hichi cha Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar na baada ya uchaguzi. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Kitaifa Zanzibar Sheikh. Salim Alkadiry akizungumza katika hafla hiyo ya Ufunguzi wa Kongamano la Kuiombea Dua Nchi kuendelea na amani Nchini lililofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein, kabla ya kumkaribisha Mlezi wa Kamati hiyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi ili kuzungumza na kumkaribisha mgeni rasmin kulifungua Kongamano hilo.
Mlezi wa Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi akizunguka katika hafla ya Ufunguzi wa Kongamano la Amani kuiombea Nchi Dua lililofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) 
WASHIRIKI wa Kongamano la kuiombea Nchi Dua ya Amani wakifuatilia Kongamano holo katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) Wilaya ya Kati Unguja wakati Mlezo wa Kamati hiyo Mhe.Balozi Seif Ali Iddi akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin kulifungua Kongamano hilo leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein akihutubia katika hafla ya Ufunguzi wa Kongamano la Amani kuitakia Nchi Amani na kuiombea Dua, Kongamano hilo limeandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya Amani Zanzibar.  






 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.