Habari za Punde

Zanzibar kuanza kuchunguza virusi vya Corona



Mkurugenzi Huduma za Uchunguzi wa Maradhi  Hospitali Kuu ya  Mnazi Mmoja  Dk.Msafiri Marijani akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uchunguzii wa virusi vya Maradhi ya Corona  huko Ofisi za Maabara kuu Mnazi Mmoja

Msaidizi Mkuu Huduma za Maabara Hospitali ya Mnazimmoja Sabra Amour akitoa maelekezo kuhusu uchunguzi wa virusi vya maradhi ya Corona  katika Ofisi za Maabara kuu Mnazi Mmoja.

Mashine ya kuchunguza Virusi vya Corona


Na Miza Kona Maelezo   

         

Wizara ya Afya Zanzibar imeanza kutoa huduma za uchunguzi virusi vya maradhi ya Corona kwa wananchi na wageni wanaoingia na kutoka nchini kwa kutumia mashine maalum ya kuchunguzia maradhi ya mripuko.


Akizungumza na Waandishi wa habari, Mkurugenzi Huduma za Uchunguzi wa Maradhi katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Dk. Msafiri Marijani amesema kifaa hicho kinauwezo wa kuuchunguza zaidi ya sampuli 90 kwa wakati mmoja na kutoa majibu masaa 24.


Ameeleza kuwa Wizara tayari imeshatoa mafunzo kwa wafanyakazi sita  kutoka kwa wataalamu walioleta mashine hiyo kwa ajili ya matumizi ya kifaa hicho hadi sasa imeshachunguza sampuli 260 na kutoa majibu sahihi.


Dk. Marijani amesema mashine hiyo pia itasaidia kuchunguza maradhi mbali mbali ya mripuko ikiwemo ebola na 

chikungunya ikiwa  yatatokezea nchini


Aidha ameishukuru Serikali na washirika wa Maendeleo kwa kusaidia  kifaa hicho na kuweza kupunguza usumbufu wa kupeleka sampuli nje ya Zanzibar.


Kifaa hicho kiliwasili nchini mwezi Mei mwaka huu kutokana na kuingia kwa mripuko wa maradhi ya Corona na kuanza kutumika mwezi huu. 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.