MENEJA wa
huduma kwa wateja wa Zantel, Fatma Mohammed Khalfan akizungumza na waandishi wa
Habari wakati uzinduzi wa duka jipya la Zantel lilipo mjini Wete eneo la Four
Ways, Kulia ni Said Masoud Ali, Meneja wa Mauzo na usambazaji Pemba, Duka hilo
litarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MENEJA wa
Maduka ya Zantel-Zanzibar,Mwajuma Hussein akionesha namna ya kutumia mfumo wa
utoaji tiketi kwa wateja (queing System) utakaorahisisha upatikanaji wa huduma
kwa wateja wanaotembelea duka jipya lililopo Wete-Pemba,Duka hilo litarahisisha
upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa wakazi wa eneo hilo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
Pemba 23, Novemba. Katika azma yake ya kuhakikisha huduma za mawasiliano
zinakuwa za uhakika, Kampuni ya Zantel imezindua duka jipya ambalo litawasaidia
wakazi wa kisiwa cha Pemba kupata huduma kwa urahisi zaidi.
Awali duka hilo lilikuwa katika eneo la Wete Sokoni na
sasa limehamishiwa eneo la Pemba Four Ways ambako ni rahisi zaidi kufikika kwa
wateja.
Duka hilo litakuwa muhimu kwa wateja wa Zantel likiwa
na kituo cha huduma kwa wateja kilichoboreshwa zaidi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkuu wa Masoko
na Huduma za Kifedha wa Zantel, Sakyi Opoku alisema uwepo wa duka hilo
utapunguza adha mbalimbali ambazo wateja walikumbana nazo awali.
“Uboreshaji wa duka hili ni sehemu ya mkakati wa
kampuni yetu wa kuhakikisha tunasogeza huduma karibu na wateja ili kuhakikisha
wanazipata huduma na bidhaa zetu kwa urahisi zaidi.”
Aliongeza “Tumehamisha duka hili kuja hapa Four Ways
ukizingatia kwamba eneo hili ni rahisi kufikika si kwa wenyeji tu bali hata
wageni.”
Duka hilo linatarajia kuhudumia zaidi ya wateja 100 likitoa
huduma mbalimbali ikiwamo usajili wa simu,huduma za kifedha (Ezypesa) pamoja na
uuzaji wa simu mbalimbali zenye uwezo wa 4G ikiwamo simu aina ya Smarta.
Duka hilo limetengenezwa kuhakikisha wateja wanapata
huduma bora ikiwamo mfumo wa kidigitali wa kusajili wateja badala ya kutumia
foleni ili kufanya huduma kuwa rahisi na haraka.
Kuhusu
Zantel
Zantel
ni Kampuni inyaoongoza kwa utoaji wa huduma za mawasiliano Visiwani Zanzibar
kwa miaka mingi hivi sasa ikiongoza kwa ubora miundombinu ya mawasiliano,
huduma pamoja na bidhaa.
Huduma
ya kifedha ya Ezypesa ni ya kwanza nchini Tanzania kutoa huduma za kibenki za
kawaida pamoja na za kiislamu kwa ushirikiano na benki ya Watu wa Zanzibar
(PBZ).
Aidha,
Zantel ni kampuni inayoongoza kwa utoaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania
kupitia uwekezaji kwenye teknolojia ya fibre optic cable
ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki na duniani
umeiwezesha Kampuni hiyo kuleta mapinduzi ya haraka ya kidigitali hapa nchini.
No comments:
Post a Comment