Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wachezaji wa Timu ya Yanga kabla ya kuaza mchezo wa Fainali ya Kombe la Mapinduzi Cup mchezo uliofanyika jana katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar Timu ya Yanga imeibuka Bingwa wa Mapinduzi Cup 2021 -2022.
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi alikuwa mgeni rasmin katika fainali za mashindano ya Kombe
la Mapinduzi ambapo Yanga SC ilitawazwa kuwa bingwa wa mashindano hayo kwa mwaka huu
2021.
Mashindano hayo ni miongoni mwa shamrashamra za sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Timu ya Yanga SC wamefanikiwa kutwaa Kombe hilo la Mapinduzi Cup baada ya ushindi wa penenti 4-3 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 za mchezo huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa Amaan, Jijini Zanzibar.
Shujaa wa Yanga SC
kwenye mchezo huo ambao mgeni rasmin alikuwa Rais Dk. Mwinyi alikuwa ni kipa Farouk
Shikaro aliyeokoa penanti ya mwisho ya Simba iliyopigwa na Mkenya mwenzake beki Joash Onyango.
Penalti za Yanga SC zimefungwa na MkongoTuisila Kisinda,
Abdallah Shaibu ‘Ninja’, Zawadi Mauya na Mrundi Said Ntibanzokiza wakati Mkongo mwingine MukokoTonombe iliokolewa na kipa Beno Kakolanya wa Simba.
Penalti za Simba SC
zilifungwa na kiungo Mkenya Francis Kahata, mshambuliaji Mkongo Chriss Mugalu na beki mzawa Gardiel
Michael, wakati mshambuliaji Mnyarwanda, Meddie Kagere na Nanodhawa Dabihiyo aligongesha mwamba wa juu wa goli kulia.
Hiyo itakuwa ni mara ya pili Yanga
SC kutwaa Kombe la Mapinduzi baada ya mwaka 2007
mashindano hayo yalipofanyika kwa mara ya kwanza ambapo waliifunga Mtibwa Sugar
kwenye fainali.
Nyota watatu wa Simba walijinyakulia tuzo baada ya mchezo huo,
Wakenya beki Joash Onyango Mchezaji Bora wa Mechi, Kiungo Francis Kahata Mchezaji Bora wa Mashindano hayo ni Mshambuliaji Miraj Athumani Mfungaji Bora kwa mabao yake manne,
Mkenya mwingine kipa Farouk Shikaro wa Yanga amejinyakulia tuzo ya Kipa Bora
kufuatia kuruhusu bao moja tu kwenye mashindano hayo.
Kikosi cha Yanga
SC kilikuwa; Farouk Shikhalo, Kibwana Shomari, Adeyoum Saleh/Paul Godfrey ‘Boxer’
dk71, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, Said Juma ‘Makapu’, MukokoTonombe,
Tuisila Kisinda, Zawadi Mauya, Michael Sarpong/Waziri Junior dk8, Said
Ntibanzokizana Haruna Niyonzima.
Simba SC;
Beno Kakolanya, David Kameta, Gardiel Kameta, Kennedy Juma, JoashOnyango,
ThadeoLwanga, Hassan Dilunga/Chris Mugalu dk61, MuzamilYassin, MeddieKagere,
Francis KahatanaMirajJuma/Ibrahim Ajibu dk72.
ViongozimbalimbaliwavyamavyasiasanaSerikaliyaMapinduziya
Zanzibar naSerikaliyaJamhuriyaMuunganowa Tanzania walihudhuriakatikamtanangehuoambapomaelfuyamashabikiwalihudhurianakujazauwanjanawenginekadhaakusalianjeyauwanja.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment