Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi Ashiriki Maziko ya Marehemu Mzee Msuri Muhidini

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wakati alipofika  katika viwanja vya Msikiti wa Muembemimba Wilaya ya Mjini Mkoa Mjini Magharibi, kushiriki  kumswalia Marehemu Mzee Msuri Muhidini aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Mjini   pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tawi la CCM Mikunguni Jimbo la Kwahani,Marehemu atazikwa  Kijijini kwao Unguja Ukuu Kaebona Wilaya ya Kati Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akijumuika na Viongozi na Waislamu kumswalia Marehemu Mzee Msuri Muhidini aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Mjini   pia aliwahi kuwa  Mwenyekiti wa Tawi la CCM Mikunguni Jimbo la Kwahani, Swala  iliongozwa na Naibu Kadhi Mkuu Sheikh Hassan Othman Ngwali (mbele)  katika Msikiti wa Muembe Mimba Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi leo,Marehemu atazikwa  Kijijini kwao Unguja Ukuu Kaebona Wilaya ya Kati Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akijumuika na Viongozi na Waislamu kuitikia dua iliyoombwa baada ya kumswalia Marehemu Mzee Msuri Muhidini aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Mjini pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tawi la CCM Mikunguni Jimbo la Kwahani,  katika Msikiti wa Muembemimba Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi leo,Marehemu atazikwa  Kijijini kwao Unguja Ukuu Kaebona Wilaya ya Kati Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) akiagana na  Waislamu na Wananchi baada ya  kumswalia Marehemu Mzee Msuri Muhidini aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Mjini na pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tawi la CCM Mikunguni Jimbo la Kwahani katika Msikiti wa Muembemimba Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi leo,Marehemu atazikwa  Kijijini kwao Unguja Ukuu Kaebona Wilaya ya Kati Unguja.

Alhaj Dk. Mwinyi alijumuika na ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi mbali mbali katika sala ya kumsalia Marehemu Mzee Msuri Muhidini huko katika msikiti wa                  Muembemimba, Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.                                                       

Alhaj Dk. Mwinyi aliwaomba wana familia kuwa na subira katika kipindi hichi kigumu cha msiba wa mzee wao Marehemu Mzee Msuri Muhidini ambaye ameacha kizuka mmoja na watoto wanne na kumuombea kwa MwenyeziMungu ailaze roho yake marehemu mahala pema peponi, Amin.

Hadi anafariki dunia Marehemu Mzee Msuri Muhidini alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Mjini ambaye pia, aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tawi la Mikunguni, Jimbo la Kwahani katika Mkoa wa Mjini Magharibi. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.