Na Rehema Kasimu, MAELEZO.
Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufanya Sensa ya Watu na Makazi
ifikapo mwezi Agosti 2022. Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Ofisi ya Taifa ya
Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar
(OCGS), ipo kwenye maandalizi ya kufanya Sensa hiyo.
Sensa
ya Watu na Makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10
ambapo Sensa ya mwisho kufanyika nchini ni ile ya mwaka 2012, sensa ya mwaka
2022 itakuwa ni sensa ya sita kufanyika nchini baada ya Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002
na 2012.
Sensa
ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathimini, kuchapisha
na kusambaza takwimu za kidemographia, kiuchumi na kijamii kuhusiana na watu
wote na makazi yao katika nchi kwa kipindi maalum, hivyo sensa ni zoezi maalum
lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsia,
mahali wanapoishi na hali yao ya elimu, hali ya ajira, hali ya vizazi na vifo
na hali ya makazi.
Takwimu
hizi za msingi ndiyo zinazoweza kuanisha mahitaji halisi ya wananchi yakiwemo
makundi maalum yenye uhitaji maalum kwa mfano, watu wenye ulemavu, wanawake,
watoto, vijana na wazee hivyo kurahisisha uandaaji wa sera na mipango ya
maendeleo kulingana na uhitaji na mazingira yaliyopo.
Umuhimu
wa kipekee wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni pamoja na kuisadia
Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia mchakato wa utekelezaji wa dira
ya Maendeleo ya mwaka 2025, mageuzi ya masuala ya afya na jamii, pamoja na
ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo za kimataifa;
Umuhimu mwingine ni pamoja na taarifa za idadi ya watu husaidia
katika mamlaka za wilaya katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo
huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye uwiano wa
mgawanyo wa rasilimali, taarifa za msingi za hali ya kidemografia, kijamii na
kiuchumi za idadi ya watu na makazi za mipango katika ngazi zote;
Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini Tanzania (NBS)
sensa ya watu na makazi ni muhimu kwa sababu inatoa tahtmini ya takwimu
zitakazosaidia kukokotoa viashiria vingine mfano pato la mtu mmoja mmoja,pato
la taifa, ajira na ukosefu wa Ajira na kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi
pamoja na taarifa itakayowezesha serikali kujua ongezeko la idadi ya watu, kwa
mgawanyo na viashiria vingine, ambavyo ni muhimu kwa usimamizi wa mazingira; na
Aidha NBS pia imesema sensa itasaidia kuleta msingi wa utawala
bora na ujumuishaji wa demokrasia. Takwimu sahihi za Sensa zinahitajika kwa
ajili ya ugawaji wa majimbo ya uchaguzi kwa ufanisi, kurekebisha mipaka ya
kiutawala katika serikali za mitaa.
Katika kuhakikisha sensa ya watu na makazi inafanikiwa nchini
Tanzania,Rais wa Jamhuri ya Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameviomba Vyombo vya
Habari kuelimisha na kuhamasisha jamii
kuhusu umuhimu wa sensa hiyo kwa kutumia
mbinu na nyenzo za kuwafikia wananchi wa
rika zote na mahali kote kupitia vipindi vya radio, televisheni ,
magazeti na Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano (TEHAMA) ya mitandao ya kijamii na jumbe za simu ili kufanikisha zoezi hilo.
Aliyasema hayo Septemba 14,
2021 wakati akizindua wa mkakati wa
uelimishaji na uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi uliofanyika Jijini Dodoma, na kuvitaka vyombo
hivyo vitenge muda na kuandaa vipindi mbalimbali vitakavyohamasisha na
kuelimisha jamii kuhusiana na zoezi hilo nchini kote ambapo pia aliwataka
Wasanii kutumia vipawa vyao katika utoaji wa elimuya sensa.
Rais Samia alieleza kuwa Sensa inaisaidia Serikali katika
kufanyaji wa maamuzi kuhusu ugawaji wa rasilimali
za taifa zikiwepo za Maji, Umeme, Afya, Elimu na Ujenzi wa Miundombinu ya huduma
za jamii, hivyo kuwataka wananchi kuhamasika na
kushiriki katika zoezi hilo ikiwa ni moja ya njia itakayotumika kutatua
chamgamoto zinazozikabili jamii zao.
“Sensa pia itatusaidiaSerikalikufanya
maamuzi katika ugawaji wa rasilimali za taifa na kupeleka hudauma mbalimbali
kwa wananchiikiwemo afya elimu maji na ujenzi wa miundombinu kwenye maeneo
mbalimbali kulingana na idadi ya watu na mahitaji ya maeneo hayo”. Alisema Rais Samia
Pia aliongezea kuwa serikali kwa sasa haina idadi kamili ya
majengo hivyo sensa itakayofanyika 2022
itahususha kuhesabu majengo ili kurahisisha zoezi la ukusanyaji wa tozo za
majengo kwa kuwa makazi ni kipimo cha
maendeleo.
“Aidha makazi ni kipimo muhimu cha
maendeleo, kama mnavyofahamu tumeweka tozo ya makazi kulipiwa kiasi fulani cha fedha, lakini
hatukuwa na idadi sahihi ya nyumba na makazi ya watanzania nchini, kwa hiyo
zoezi hili litakwenda kutupa ubora na
kujiamini kuwa tunafanya kazi kwa kujua idadi ya nyumba zilizopo”. Alisema Rais Samia
Pamoja na hayo Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Mwigulu Nchemba alieleza dhumuni la mkakati wa uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi kuwa ni kukabiliana na mila na fikra potofu
ambazo zitaweza kukwamisha zoezi hilo, hivyo kabla ya sensa kuanza ni muhimu watu wapewe mafunzo kuhusu zoezi hilo.
Alibainisha kuwa Serikali imeshatoa maelekezo ya fedha zitakazotumika
kuratibu na kusimamia shughuli zote za sensa ya Watu na Makazi ili kuwezesha ukusanyaji wa taarifa hizo kwa ufanisi, na matokeo ya sensa hiyo ni
dira ya Wizara ya fedha kupanga mikakati ya kimaendeleo kwa wananchi.
Aidha Mtakwimu Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Ofisi ya Taifa ya
Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa, alifafanua
kuwa sensa itakayofanyika mwaka 2022, itakuwa ya kipekee kuwahi kufanyika miongoni mwa zote tano
zilizowahi kufanyika tangu uhuru kwani walitumia teknolojia ya makaratasi kwa
asilimia 95 na ya mwaka 2012 walitumia teknolojia ya scanning ambayo ilitoa matokeo
ndani ya miezi 3 Hivyo sensa ya mwakani itatoa matokeo ndani ya mwenzi mmoja.
Alisema katika sensa tano zilizopita uchambuzi uliishia katika
ngazi ya Wilaya, hivyo sensa itayofanyika mwakani itahusisha ngazi za Kata,
Vijiji na Vitingoji ambapo watu na
majengo yao vitahesabiwa nchini kote na
anwani ya kila makazi kurekodiwa kwenye Kazi Data ya Taifa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment