Habari za Punde

Waandishi wa Habari Pemba Wapatiwa Mafunzo Kuhusu Uongozi Kwa Wanawake.

MRATIBU wa mradi wa ushirikishaji wanawake katika uongozi kutoka TAMWA ZNZ, Salma Amir Lusangi akifungua mafunzo ya siku tatu kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali Pemba, mafunzo hayo yalioandaliwa na TAMWA Zanzibar Ofisi ya Pemba, chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Norway nchini
KAIMU meneja wa Radio Jamii Mkoani Said Omar Said, akiwasilisha majibu wa kundi namba mbili wakati wa mafunzo ya waandishi wa habari juu ya kuwajengea uwezo na ufahamu, taratibu za ufuatiliaji wa matumizi ya mali za umma, ushawishi Pamoja na utetezi wa masilahi ya umma, mafunzo yaliyofanyika Ofisi za TAMWA Zanzibar Ofisi ya Pemba
MRATIB wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said, akizungumza wakati wa mafunzo ya siku tatu kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali Pemba, mafunzo hayo yalioandaliwa na TAMWA Zanzibar Ofisi ya Pemba, chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Norway nchini.

BAADHI ya waandishi wa habari kutoka Vyombo mbali mbali vya habari Pemba, wakifuatilia kwa makini mafunzo ya siku tatu juu ya mradi wa ushirikishaji wanawake katika uongozi, mafunzo hayo yalioandaliwa na TAMWA Zanzibar Ofisi ya Pemba, chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Norway nchini.

(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.