Habari za Punde

Kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar ziarani Pemba

AFISA utawala wa Hoteli ya The Manter Resort Zamda Hussein (katikati), akitoa maelezo juu ya mifumo ya usajili wa wageni na utoaji wa risiti za kielektroniki kwa wateja baada ya kupata huduma katika hoteli hiyo, kwa wajumbe wa kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kulia mwenyekiti wa kamati hiyo Sabiha Filfil Thani na kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Jamal Kassim Ali.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

AFISA utawala wa Hoteli ya The Manter Resort Zamda Hussein, akionyesha mashine ya utoaji wa Risiti za Kieletronik (VFMS)jinsi zinavyofanya kazi katika uingizaji wa taarifa za wageni, kwa wajumbe wa kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kulia mwenyekiti wa kamati hiyo Sabiha Filfil Thani na kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Jamal Kassim Ali.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MWENYEKITI wa kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Sabiha Filfil Thani, akiangalia jinsi mashine ya utoaji wa risiti za Kieletronik (VFMS) inavyofanya kazi, kushoto ni Afisa utawala wa Hoteli ya The Manter Resort Zamda Hussein, wakati wajumbe wa kamati ya Uchimi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar ilipotembelea hoteli hiyo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

KAMISHNA wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Salum Yussuf Ali, akitoa ufafanuzi wa maswali ya wajumbe wa Kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, walipotembelea hoteli na kukagua mifumo ya utoaji wa Risiti za kielektroniki.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKURUGENZI wa Mifumo ya kimtandao kutoka ZRB (IT) Harith Abdilazizi Ahmada, akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, juu ya ufanyaja kazi wa mashine za utoaji wa risiti za kielektronik zinavyofanya kazi na ZRB wanavyoona kila kinachofanyika.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

WAJUMBE wa kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakiwasili katika hoteli ya The Aiyan, kwa ajili ya kluangalia mifumo ya kisasa ya utoaji wa Risiti za Kieletronik katika hoteli hiyo, wakiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Sabiha Filfil Thani na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha, Mipango Zanzibar Jamal Kassim Ali na Kamishana ZRB Zanzibar Salum Yussuf Ali.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

MWENYEKITI wa Kamti ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Sabiha Filfil Thani(kulia), akifuatiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Jamal Kassim Ali, wajumbe wa kamati ya uchumi Nadir Abdullatif Yussuf na Ameir Abdalla Ameir, wakisikiliza maelezo kutoka kwa meneja Mkuu wa Hoteli ya The Aiyan.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.