MDHAMINI wa Kamisheni ya Utalii Pemba Hamad Amini
Ali, akizungumza na wanafunzi wa skuli ya Madungu Sekondari, baada ya kufanya
usafi katika fukwe ya Shamiani Mwambe, kwa lengo la kutangaza fukwe hiyo kuwa
kivutio cha utalii ndani ya kisiwa cha Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
BAADHI ya wanafunzi wa skuli ya Madungu Sekondari
wakifanya usafi katika Ufukwe wa Kisiwa cha Shamiani Mwambe, ikiwa ni lengo la
kuutangaza Ufukwe huo kuwa kivutio cha utalii Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WANAFUNZI wa Skuli ya Madungu Sekondari wakizoa taka
baada ya kufanya usafi katika ufukwe wa Kisiwa cha Shamiani Mwambe, ikiwa ni
mikakati ya kutangaza ufukwe huo kuwa kivutio cha Utalii Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MIONGONI mwa Fukwe bora, kubwa na safi Kisiwani
Pemba kwa sasa ni Ufukwe wa Kisiwa cha Shamiani Mwambe, ikiwa ni moja ya
vivutio vikubwa vya utalii ndani ya Kisiwa cha Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
No comments:
Post a Comment