Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Familia ya Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Ahmed Nassor Mazrui alipowatembelea nyumbani kwao Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kuwafariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wao kwenye ajali ya Ndege.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala Mabodi na Familia yake, alipomtembelea nyumbani kwake Chukwani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kumfariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wake kwenye ajali ya Ndege.
No comments:
Post a Comment