Habari za Punde

MIRADI INAYOTEKELEZWA ZANZIBAR NI MATUNDA YA MUUNGANO

 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Mitawi akitoa maelezo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza wakati hafla ya makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Mitawi  akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla mkataba wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi
Katibu Mkuu Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Bw. Thabit Idarous Faina na Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Bi. Farhat Ali Mbarouk wakisaini mkataba wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akishuhudia Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hamis Mitawi akitia saini mkataba wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi leo Aprili 29, 2022. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Bw. Dustun Shimbo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba kwa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais iliyogfanyika iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema utekelezaji wa miradi upande wa Zanzibar ni matunda ya ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

Amesema hayo wakati wa hafla ya utiaji saini wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba kwa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi ambapo mradi huo utatekelezwa na Kampuni ya Dezo Civil Contractors Co. Limited.

Mhe. Hemed alisema kuwa SMZ inafarijika kuona mradi huo unaanza kutekelezwa kwa vitendo na kwamba utaleta manufaa makubwa kwa wananchi watakaonufaika na mradi huo.

Pia alitumia nafasi hiyo kutoa pongeza na shukrani kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango pamoja na Ofisi yake kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa SMZ.

Awali akitoa taarifa kuhusu mradi huo Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Bi. Mary Maganga, alisema tathmini katika ufukwe wa Sipwese ilionesha kuwa maji ya bahari yameingia katika maeneo ya kilimo cha mpunga na wananchi wa Shehia ya Mkungu, Kijiji cha Sipwese eneo la kwa Mgogo.

Mitawi alisema kujaa kwa maji haya pia yamesababisha kukatika kwa mawasiliano kutoka upande wa pili takribani kilometa 3.360 ambako ndiko wananchi wanafuata huduma za jamii kama vile shule hali inayosababisha watoto wa shule kuvuka maji shingoni kuweza kuifikia shule. 

“Mmomonyoko wa fukwe zilizo katika Bahari ya Hindi kwa upande wa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani umeendelea kuwa ni changamoto katika maeneo mengi ya fukwe na umeanza kuleta athari katika baadhi ya maeneo kwa kusababisha uharibifu wa miundombinu iliyopo kama vile barabara, majengo, makazi ya watu na madaraja.

 

“Hali hii imesababisha Serikali kutumia fedha nyingi katika kukarabati miundombinu iliyoharibiwa, Fedha ambayo ingeweza kupelekwa katika maeneo mengine muhimu kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijami,” alisema Mitawi.

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.