Habari za Punde

Wadau wa masuala ya kilimo waishauri jamii kutumia vyakula vinavyozalishwa na mbolea asili kuepuka maradhi

 

Mkuu wa kitengo cha utafiti na tathmini kupitia mradi wa Viungo Ali Abdalla alipokua akieleza namna ya hali halisi ilipofikia ya utekelezaji wa mradi huo.

Miongoni mwa wajumbe wa kamati hiyo ya Uashauri wakifuatilia kwa umakini uwasilishwaji wa taarifa za utekelezaji mradi huo.

Na Muhammed Khamis


Kamati ya ushauri ya utekelezaji wa mradi wa VIUNGO Zanzibar (ZMAG) imesema jamii visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla inaweza kuepuka maradhi mbali mbali iwapo wataacha kutumia vyakula vinavyotumia mbolea ya kemikali wakati wa uzalishwaji wake na kutumia vyakula vinavozalishwa kwa kupitia  mbolea za asili wakati wa uzalishaji wake (Organic food.)


Ushauri huo umetolewa na wajumbe wa kamati  ya ushauri na wadau mbalimbali wa masuala ya kilimo wakati wa kikao cha kuangalia ni namna gani mradi VIUNGO unaendelea kutekelezwa na kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo cha mbogamboga,matunda na viungo ili kuleta tija kwa pande zote.


Mkutano huo uliofanyika katika ofisi za wizara ya kilimo  Maruhubi Zanzibar na kuwashirikisha wadau kutoka taasisi tofauti zikiwemo za Seikali, mashirika yasio ya kiserikali na wakulima .


Wakichangia mada zilizowasilishwa katika mkudano huo ndugu Ali Abdalla kutoka……. alisema kuna idadi kubwa ya wananchi kwenye jamii bado hawajaelewa umuhimu wa kutumia vyakula vinavozalishwa na  mbolea asili na ndio maana hadi leo wananchi walio wengi huendelea kutumia vyakula vinazozalishwa kwa kutumia kemikali jambo ambalo ni hatari sana kwa afya na ardhi.


Alisema tafiti mbali mbalimbali zinazonesha watu wengi hupata maradhi tofauti na imebainika kuwa chanzo cha maradhi hayo ni kutumia vyakula ambavyo uzalishwaji wake hutumia mbolea nyingi zisizokua za asili na ndio chanzo cha matatizo mengi hivi sasa.


Alieleza kuwa licha ya kuwa suala la uelewa ni tatizo linalosababisha wananchi kutumia bidhaa hizo lakini pia alisema baadhi yao hufuata urahisi wa bidhaa zinazozalishwa kupitia mbolea ya kemikali ukilinganisha na mbolea za asili ingawa alisema hazofautiani sana ukichunguza kwa undani.


Katika hatua nyengine mtalamu kutoka wizara ya kilimo Zanzibar Omar  Abuubakari alisema wakulima wengi Zanzibar na Tanzania wamekua wakiendenlea kutumia mbolea za kemikali kwa kile wanachokiamini kwamba uzalishaji mkubwa zaidi wa mazao yao kinyume na matumizi ya mbolea za asili.


Alisema kwa mazingira hayo jitihada  zaidi zinahitajika ikiwemo utoaji wa elimu kwa jamii  ili iweze kutambua umuhimu wa kutumia chakula kilichozalishwa kwa kutumia mbolea za asili.


Kwa upande wake Dkt.Mzuri Issa alisema wakati wanaendelea kufikiri kuhusu hali hiyo  kuna umuhimu mkubwa kutazama pande zote mbili ukizingatia mbolea za kemikali ni biashara ambayo inategemewa na wengi.

 

Alisema suala muhimu zaidi ni jamii kupewa elimu ili waweze kufahamu madhara ya utumiaji wa vyakula vinavyozalishwa kwa kutumia mbolea za kemikali na kuoneshwa faida za kutumia mbolea za asili.


Akifafanua zaidi alisema anaamini kupitia mfumo huo utaweza kutoa elimu kwa kina na kuwaacha wananchi kuamua wenyewe ni mazao gani wanahitaji kutumia katika maisha yao ya kila siku.


Akieleza kuhusu baadhi malengo ya mradi wa VIUNGO meneja mkuu wa mradi huo wa VIUNGO Amina Ussi khamis alisema ni kuwawezesha wakulima Unguja na Pemba kupitia njia bora za kilimo.


Pia alisema ni kuwainua  baadhi ya akina mama ambao ni wanufaika wa mradi huo ikiwemo kuwapa elimu ya kuwanzishwa kwa vikundi vya kuweka na kukopa ili waweze kukidhi shughuli zao za kila siku.


Aidha alisema malengo mengine ni kufungua fursa kupitia mnyororo wa thamani kutoka kwa wakulima hadi kwa mlaji,  ambapo anaamini kuwa una fursa nyingi ambazo zinaweza kuingiza kipato kwa kila mtu ambae ni mnufaika wa mradi huo.


Mradi wa VIUNGO ni wa miaka minne ambao umelenga kuwafikia wanufaika zaidi ya 57,000 kwa Unguja na Pemba na unaotekelezwa na taasisi tatu ikiwemo People Development Forume,Community Forest in Pemba (CFP) pamoja na Tanzania Media Women Association TAMWA-ZNZ  kwa ufadhili Jumuia ya Ulaya (EU)


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.