Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Amerejea Nchini Akitokea Nchini Burundi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akiteremka ndege ya  katika  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akiwa na  Mkewe Mama Mariam Mwinyi pamoja na Maafisa mbali mbali akitokea katika nchi ya   Burundi kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mama Samia Suluhu Hassan katika sherehe za maadhimisho  ya miaka 60 ya nchi hiyo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama Zanzibar, alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akiwa na  Mkewe Mama Mariam Mwinyi, akitokea  Nchi ya   Burundi kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mama Samia Suluhu Hassan katika sherehe za maadhimisho  ya miaka 60 ya nchi hiyo. 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amerejea nchini leo akitokea Burundi ambapo alihudhuria sherehe za miaka 60 ya Uhuru wa nchi hiyo.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Rais Dk. Mwinyi alipokewa na viongozi mbali mbali wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah.

Rais Dk. Mwinyi ambaye alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika safari yake hiyo alifuatana na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo mkewe Mama Mariam Mwinyi.

Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano,

Ikulu Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.