Habari za Punde

Serikalo Imejipanga Kuongeza Uzalishaji Sekta ya Uvuvi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa kwanza kushoto) akizindua jengo jipya  na kulikabidhi kwa Kikundi cha Ulinzi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi cha Dunda katika hafla fupi iliyofanyika Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani Julai 5, 2022. Wengine pichani ni Wabunge na Viongozi mbalimbali wa Mkoa huo.

Mratibu wa Mradi wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFish), Bw. Nichrous Mlalila (kushoto) akitoa maelezo kuhusu jengo jipya la Kikundi Shirikishi cha Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi cha Dunda (BMU) kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) muda mfupi baada ya Waziri huyo kuzindua jengo hilo ili litumike kwa kazi ya kulinda  rasilimali hizo Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallah(kushoto) akimueleza jambo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki katika hafla fupi ya kuzindua na kukabidhi jengo jipya kwa Kikundi cha Ulinzi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi cha Dunda(BMU) iliyofanyika Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani 

Na Mbaraka Kambona, Pwani

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema Serikali imejipanga kuwawezesha Wavuvi vifaa vya kisasa ikiwemo boti  kwa lengo la kuwaweze  kuvua  samaki  kwenye kina kirefu ili  waongeza uzalishaji wa samaki, kuinua  uchumi wao  na kukuza pato la  taifa.

Ndaki alibainisha hiyo wakati wa hafla fupi ya kuzindua na kukabidhi jengo jipya kwa Kikundi Shirikishi cha Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi cha Dunda (BMU) kwa ajili ya kuimarisha ulinzi  wa rasilimali za  bahari katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi iliyofanyika Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani Julai 5, 2022.

Alisema kuwa Serikali inataka kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi na ndio maana Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameongeza bajeti ya Sekta ya Uvuvi ya Mwaka 2022/2023 ambapo sehemu yake itatumia kununua boti zaidi ya mia tatu (300) ili wakopeshwe wavuvi kwa lengo la kuboresha shughuli zao.

Aliongeza kwa kusema kuwa boti hizo zitasaidia wavuvi kwenda katika kina kirefu na kuvuna mazao mengi ya samaki na kufanya viwanda vya kuchakata samaki kufanya kazi kwa uwezo wake tofauti na ilivyo sasa ambapo viwanda vingi vinafanya kazi chini ya uwezo uliosimikwa.

Aidha, Waziri Ndaki aliwataka wananchi kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupiga vita uvuvi haramu huku akisisitiza kuwa kazi hiyo siyo ya Wizara ya Mifugo na uvuvi peke yake bali ni ya kila mmoja.

"Samaki ni lishe, samaki ni pesa, samaki ni biashara na samaki ni ajira, tushirikiane kupiga vita uvuvi haramu," alisema

Halikadhalika aliwataka Viongozi wa Vikundi Shirikishi vya Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi kuwa waadilifu na kujiepusha na vitendo vya rushwa na upendeleo kwani ndio chanzo cha  uvuvi haramu.

Kwa upande wake,  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mhe. Zainabu Abdallah aliishukuru serikali kwa namna ilivyojipanga kuwawezesha wavuvi  akiamini kuwa kwa mipango hiyo ya Serikali Wavuvi katika Wilaya yake watanufaika kupitia shughuli zao hizo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.