Na.Mwandishi wa OMKR.
Imeelezwa kwamba kuanza kwa hatua za ujenzi Bandari Rasmi katika Kijiji cha Shumba mjini Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba ni utekelezaji wa mipango ya serikali ya Kukifungua kisiwa cha Pemba katika fursa mbali mbali za kiuchumi na kimaendeleo.
Hayo yameelezwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, alipotembelea kukagua na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Bandari rasmi huko katika kijiji hicho kilichopo wilaya ya Micheweni Pemba.
Amesema kwamba Zanzibar imedhamiria kuona kwamba kisiwa cha Pemba kinafunguka kiuchumi kwa kuwepo na kuendelezwa fursa mbali mbali za kibiashara zitakazochangia pato la wananchi na kuchangia kukuza uchumi wa Zanzibar.
Amesema kwamba bandari hiyo itakapokamilika mbali na kuwasaidia sana wakaazi wa kisiwa cha Pemba hasa wa Kijiji cha Shumbamjini lakini itasaidia sana kuimarisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Zanzibar.
Mhe. Othman amesema kutokana na
umuhimu wa Bandari kibiashara na kiuchumi tayari baadhi ya wafanyabiashara
kutoka Kenya wameanza kufika Kisiwani humo kuona fursa za kibiashara
zitakazopatikana kupitia ujenzi huo wa bandari itakapokamilika mwazi Oktoba
mwakani.
Ameitaka Kampuni iliyopewa kazi
hiyo kuhakikisha kwamba wanakamilisha ujenzi huo wa Bandari kama ilivyokubali
itakapo fika mwezi wa Oktoba mwaka ujao.
Aidha amewataka wananchi wote hasa
wa eneo hilo kuhakikisha kwamba wanatoa mashirikiano ya kutosha na Mkandarasi
anayejenga Banadari hiyo ili kazi iliyokusudiwa ikamilike kwa wakati na tija
kwa wananchi na Zanzibar kwa ujumla iweze kupatikana.
Mapema Mkurugenzi wa Ufundi wa
Shirika la Bandari Zanzibar Ndugu Salum Udi amemueleza Mhe.Othman Masoud kwamba
shughuli zinazoendelea katika ujenzi huo ni kazi za kitaalamu ambazo
zimekamilika na kwamba michoro ya bandari hiyo ipo tayari na itapeleka kwa wadau
kwa ajili ya kufanyiwa mapitio ili kazi rasmi iweze kuanza.
Alifahamisha kwamba miongoni mwa
kazi nyengine zilizofanyika ni pamoja
uchuguzi wa udongo , kupima kupima kina chama maji na kwamba imebaini
kwamba ujenzi huo utafanyika kwa njia ya tuta
badala ya mfumo mwengine wa ujenzi wa bandari.
Amesema ujenzi wa bandari hiyo
yenye urefu wa mita 40 kwa ishirini
itakapokamilika itakuwa na uwezo wa
kutia ndanga meli zenye ujazo wa mizigo ipatayo tani 2000 na inatarajiwa
kukamilika Oktoba 2023.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini
Pemba Salama Mabarouk Khatib , amemueleza Mhe. Makamu kwamba viongozi wa mkoa
huo kwa kushirikiana na wananchi na wadau ,mbali mbali watahakikisha kwamba
kazi hiyo inakamilika kwa wakati ulipangwa na wananchi waweze kunufaika.
Mapema Mhe. Makamu alijumuika na
waumini wa Dini ya Kiislamu Katika ibada
ya swala ya ijumaa huko masjid Likadim Shumba mjini ambapo aliwataka waumini
hao kuendelea na juhudi ya malezi bora kwa vijana ili kuzuia upotevu wa
uadilifu na maadili uliopo hivi sasa ndani ya jamii.
Amesema kwamba visiwa vya Zanzibar
hivi sasa vimekumbwa na janga kubwa la ukosefu wa uadilifu na hivyo kuwafanya
vijana kutamani kupata kwa njia yoyete hata zikiwa ni za dhulma.
Mapema Khatib wa swala ya Ijumaa
katika msikiti huo Sheikh Haji Masoud
Kombo amewakumbusha waislamu kuhakikisha wanatekeleza kwa vitendo maamuru ya
mwenyezimungu kwa kuwa huko ndio kumcha mungu Muumba.
No comments:
Post a Comment