Na. Mwandishi OMKR
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka wanajamii na watendaji mbali
mbali kubadilika na kuchukua hatua za ziada katika kupambana na uhalifu unaojitokeza katika maeneo mbali mbali
nchini.
Mhe. Othman ameyasema hayo
alipofika kuifariji Familia ya
Mfanyabiashara maarufu nchini Said Salim Bakharesa kufuatia kifo cha
mwanafamilia Salim Ahmed Salim Bakharesa, ambaye alivamiwa na kujeruhiwa kwa visu na watu wasiojulikana na kusababisha kifo akiwa hopitalini nchi
Afrika ya kusini alikopelekwa kwa
matibabu.
Mhe. Othman amesema kwamba
watendaji wa vyombo mbali mbali hawanabudi kutambua kwamba mji wa Zanzibar
umekua na tabia na miendo ya watu kubadilika sana na kwamba lazima wachukue
hatua sahihi na za zaidi kutokana na mabadiliko hayo yaliyopo.
Amesema uhalifu unaojitokeza katika
maeneo mbali mbali unatokana na kubadilika kwa tabia za wanajamii sambamba na
kuongezeka watu wenye hulka tofauti jambo linalochangia kujitokeza vitendo
vingi vya uhalifu hapa nchini.
Amesema kwamba wanajamii na
wasimamizi wa sheria nchini wanahitaji kuwa
na mtazamo mwengine na kubadilika katika utendaji wa kazi zao na kuyatazama masuala mbali mbali kiutendaji
kwa upana zaidi kuliko ilivyo sasa ili kukabiliana nayo kwa usahihi na uhakika.
Amesema kwamba tabia mseto
zinazojitokeza Zanzibar zinachangia sana kuwepo matukio ya aina mbali mbali ya
uhalifu jambo linalohitaji watendaji kufanya kazi ya ziada katika kupambana na
hali hiyo isiendelee nchini.
Amefahamisha kwamba jamii na vyombo
mbali mbali vya utendaji vinahitaji kufanya marekebisho ya utendaji wao ili
kuwa na mbinu bora na za kisasa katika kukabiliana na uhalifu wa aina
mbali mbali nchini.
Amefahamisha kwamba licha ya serikali kujitahidi kuweka mikakati imara katika kupambana na masuala mbali mbali
yakiwemo ya uhalifu na hasa udhalilishaji, lakini masuala hayo yamekuwa yakiongezeka kutoka na mji kukua na idadi ya watu kuongezeka na kwamba mabadiliko
ya kiutendaji ni jambo linalohitajika sana katika maeneo yote.
Mhe. Othman aliitaka familia hiyo kuendelea kuwa na subra na ustahamilifu
katika kipindi kigumu cha msiba wa kuondokewa na mwanafamilia wao na kuendelea
muombea dua marehemu ili kupata msamaha wa mola muumba.
Naye mwanafamilia hiyo Ahmed Salim
Bakharesa amesema kwamba kuna haja kubwa kwa serikali kufikiria kuweka mkazo na
kuipa nguvu zaidi poliisi jamii ili isaidie vyema katika kukabiliana na vitendo
vya uhalifu wa aina mbali mbali nchini.
Marehemu Salim Ahmed Salim
Bakharesa, aliyevamiwa na watu wasiojulika nyumbani kwake na kujeruhuiwa kwa
kisu wiki chache zilizopita alipelekwa
kwatika Hospitali Hill Park Mjini Johanasbag Afrika kusini ambako alifariki na
kuzikwa jana .
No comments:
Post a Comment