05 Januari, 2023
MAKAMO
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaahidi vijana kushirikiana nao katika
kufanyana kazi za ujenzi wa maendeleo ya nchi.
Alisema vijna ni nguzo muhimu katika kusukuma mbele
maendeleo ya uchumi wa taifa ndio sababu ya serikali za SMZ na SMT zimeteua vijana wengi kushika nafasi
mbalimbali za uongozi ili kuwapatia uzoefu wa kuongoza nchi yao kwa uwezo na
weledi wa kuchapa kazi na kuijenga nchi kiuchumi na maendeleo.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo huko viwanja vya Mnara wa
Kisonge, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi wakati wa shehere za uzinduzi
wa matembezi ya vijana ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za miaka 59 ya Mapinduzi
ya Zanzibar ambayo kilele chake ni Januari 12, mwaka huu.
Dk. Mwinyi alieleza kuwa vijana wana nafasi kubwa ya
kutumikia taifa lao na kuliletea maendeleo sambamba na kuwaasa vijana hao
kwamba wanapaswa kujitambua kwa kujiweka imara ili kufanikisha malengo ya
ukombozi wa kweli kwenye jamii zao.
“Kama nyote mnafahamu kwamba Nchi yetu ilipata uhuru
tarehe 12 Januari mwaka 1964, kwa njia ya kufanya Mapinduzi ambayo kwa kiasi
kikubwa yaliendeshwa na vijana wakati huo” alithimlia Dk. Mwinyi.
Aidha, aliwaeleza kwamba kazi iliyo mbele yao ni kujenga
nchi baada ya kupata uhuru pamoja na kuwakumbusha kwenye suala muhimu la
kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamamo katika jamii ambayo ndio chachu
ya maendeleo ya nchi ilipofikia
Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuwashauri vijana hao kushikamana
na kusaidiana katika kutafuta na kujitengenezea ajira ili kujitatulia
changamoto mbalimbali zinazowakabili katika kujitafutia maenedeo.
“Tambueni Serikali yenu ya awamu ya nane inaunga mkono juhudi zenu zinazofanikisha kuondoa changamoto za ajira nchini na kujiletea
maendeleo katika jamii zenu” alitanabahisha Dk. Mwinyi.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria
kuweka mazingira wezeshi kwa makundi yote ya vijana kwa lengo la kuwapatia
fursa za ajira vijana kwa namna yoyote iliyobora na sahihi kwa mijibu wa sheria
na taratibu za nchi.
Akizungumzia suala la vikundi vya maendeleo ya vijana,
Dk. Mwinyi aliwaahidi kwamba serikali itawapatia mikopo kwaaajili ya kuendeleza
juhudi zao za maendeleo na kueleza kuwa atazisimamia mamlaka husika ili ziwape
vijana kipaumbele kwenye wepesi wa kupata mikopo ili wanufaike na mipango ya serikali ya
kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Alisema serikali zote mbili za SMZ na SMT zimeweka mifumo mizuri ya
kuwawezesha vijana kupata ajira kupitia sekta za umma na binafsi, mifumo
aliyoieleza kwamba imewaepusha vijana kuepukana na mambo maovu, kuwajenga vijana
kuwa wazalendo raia wema kwa taifa lao na kuwafanya vijana kujiona fahari
kufanya kazi za kujitolea katika kujiletea maeneleo ya nchi yao.
“Nyinyi Umoja wa vijana wa CCM mna dhima kubwa ya
kuwaongoza na kuwaelekeza vijana wenzenu kuwa na maono hayo” DK. Mwinyi aliwashauri
vijana hao.
Dk. Mwinyi aliwataka vijana kutumia mbinu tofauti kwa
kuwafundisha vijana wenzao jinsi ya kuwa wazaleo kwa kujiepusha kujiingiza
kwenye vitendo viovu ikiwemo matumizi ya dawa za kulenya, udhalilishaji na vitendo vyote vya uvunjifu wa sheria za
nchi.
Akizungmza kwenye hafla hiyo, Mlezi wa Umoja wa Vijana wa
CCM, Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Maryam Mwinyi aliwaasa vijana hayo kuzidisha
nidhamu kwenye kutumikia chama chao na kuwaomba kuendelea kuisemea vizuri
serikali yao na juhudi za maendeleo zinazofanywa na chama chao.
Aidha, akiwaasa kuendelea kuchukua tahadahari kwenye
jamii zao kwani bado ugonjwa wa korona upo duniani na Zanzibar ni kisiwa chenye
mchanganyiko wa watu kutoka mataifa mengi hiyo aliwaomba vijana hao
kushajihisha umuhimu wa chanjo ili kujinusuru sambamba na kuwaasa kuendelea
kupiga vita dhidi ya udhalilishaji wa wanawake na watoto ilikujenga jamii iliyo
bora.
Mapema akizungumza kwenye hafla hiyo, Naibu Katibu Mkuu
wa CCM, Dk. Abdalla Juma Mabodi aliwaasa vijana hao kuhubiri maridhiano ya nchi
ili kudumisha jamii yenye umoja na mshikamano katika kujenga taifa lenye
maendeleo ya amani na utulivu.
Alisema Chama Cha mapinduzi daima kinaungamkono juhudi za
serikali na lazima kifuate maagizo na maono ya viongozi wa nchi.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM taifa, Mjumbe wa
Kamati ya Halmashauri kuu taifa, Komredi Muhammed Ali Kawaida, alisema vijana
watatumia fursa iliyotolewa na serikali ya kufanya mikutano ya hadhara kwa
kuyasemea mazuri yote zanayofanywa na serikali za SMZ na SMT na kwamba chama
chao cha CCM kitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali mbili
hizo.
Matembezi hayo ya vijana yataendelea kwa siku saba
mfululizo yenye kauli mbiu yake “Uchumi wa buluu kwa maendeleo ya viwanda,
vijana tuachangamkie fursa” yanajumuisha shughuli mbambali za ujenzi wa taifa.
No comments:
Post a Comment