Na. Benedict Mlawa wa Jeshi la Polisi
Jeshi la Polisi
kupitia Mtandao wa Polisi Wanawake Tanzania (TPF-NET) limeshiriki katika kuadhimisha sherehe ya
siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika Machi 08, 2023 Wilayani Kondoa Jijini Dodoma.
Maadimisho hayo yameongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule leo Machi 08,
2023 ambaye ameongoza
viogozi wa Kiserikali, Chama, Vyombo vya Ulinzi na Usalam, Taasisi ,
Mashirika, Dini Pamoja na Wananchi katika kuadhimisha ya siku ya Wanawake
Duniani ambayo imefanyika kimkoa
Wilaya ya Kondoa Jijini
Dodoma, ambapo maadhimisho haya
yamebebwa na kauli mbiu isemayo “Ubunifu na Mabadiliko ya Technolojia, chachu
katika kuleta Usawa wa Kijinsia”
Mkuu wa Mkoa aliwashukuru na kuwapongeza viongozi na wakazi
wa Wilaya ya Kondoa kwa maandalizi mazuri
waliyoyafanya kwa kuupokea ugeni mzima wa mkoa wa Dodoma katika wilaya yao.
Pia, Senyamule alisema anamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Daktari Samia
Suluhu Hassan kwa kuwa chachu ya mafanikio kwa Wanawake hapa nchini kwa kuamini kwamba Wanawake
wanaweza hata ukiangalia katika uteuzi wake waviongozi wanawake wamepewa nafasi kwa kuamini usawa wa Kijinsia.
Hata hivyo, Mkuu wa
Mkoa Rosemary Senyamule aliwa taka wanawake kujitokeza na kuzifanyia kazi fulsa
mbalimbali ambazo zinatolewa
serikali ili kuweza kufikia malengo ya
Usawa wa Kijinsia kwa maendeleo endelevu.
Pia, Mkuu wa Mkoa
Rosemary Senyamule aliongeza kwa kusema Jamii lazima izingatie haki za watoto
wa kike kwa kumlinda mtoto wa kike dhidi
ya ndoa za utotoni ili aweze kufikia na kufaidi huduma za jamii ikiwa ni
pamoja na kupata elimu yenye kuwezesha kudai na kumlinda mtoto wa kike
dhidi ya Ukatili wa Kijia.
Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa Rosemary Senyamule aliwatunuku
zawadi wanafunzi mbalimbali wa Wilaya
zote za Jiji la Dodoma waliofanya vizuri kwa kupata ufaulu wa (DIVISION 1) katika mitihani yao ya Mwisho
ya kidato cha nne mwaka 2022.
No comments:
Post a Comment