Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia
Suluhu Hassan akimkabidhi Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt.
Peter Mathuki Hati ya Umiliki wa Ardhi yenye ukubwa wa ekari 125 bure bila
malipo yoyote kwa ajili ya Jumuiya hiyo mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika
Ikulu Ndogo ya Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Biashara la Afrika
Mashariki (EABC) John Bosco Kalisa Hati ya umiliki wa Ardhi yenye ukubwa wa
ekari 3 bure bila malipo yoyote kwa ajili ya Baraza hilo Jijini Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akimkabidhi Mwanachama Mkazi wa Baraza la Chama cha Wanasheria wa
Afrika Mashariki (EALS) Moses Mahuna Hati ya umiliki wa Ardhi yenye ukubwa wa
ekari 5 bure kwa ajili ya matumizi ya Chama hicho cha Wanasheria kwenye hafla
fupi iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akimkabidhi Katibu Mtendaji wa Chama cha Udhibiti wa Nishati kwa
Afrika Mashariki Geoffrey Mabea Hati ya umiliki wa Ardhi yenye ukubwa wa ekari
4 kwa ajili ya matumizi ya Chama hicho katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu
Ndogo ya Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC) Dkt. Peter Mathuki wanne kutoka (kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax watano kutoka (kulia),
Mwakilishi kutoka Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS) Moses Mahuna
watatu kutoka (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Biashara la Afrika
Mashariki (EABC) John Bosco Kalisa wanne kutoka (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Arusha
Mhe. John Mongella watatu kutoka (kulia) pamoja na Katibu Mtendaji wa Chama cha
Udhibiti wa Nishati kwa Afrika Mashariki Geoffrey Mabea wa kwanza (kulia)
kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax pamoja na Naibu Waziri wa Wizara hiyo
Mhe. Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk mara baada ya kukabidhi Hati ya Umiliki wa
Ardhi kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika Ikulu Ndogo ya Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa
kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella mara baada
ya kukabidhi Hati ya Umiliki wa Ardhi kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
katika Ikulu Ndogo ya Arusha tarehe 03 Machi, 2023.
PICHA NA IKULU.
No comments:
Post a Comment