Habari za Punde

Wanawake NEC Wakabidhi Msaada Gereza Kuu la Isanga Dodoma

Mwenyekiti wa TUGHE tawi la Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Nuwia Sultan (kulia aliyeshika boksi) akikabdhi msaada wa vitu mbalimbali kwa Msaidizi wa Gereza la Wanawake Isanga, Mrakibu Msaidizi wa Magereza Yuster Ligazio wakati wanawake watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi walipowatembelea Gereza Kuu Isanga Dodoma na  kukabidhi msaada huo kwaajili ya  wafungwa, mahabusi wanawake na watoto wao katika Gereza hilo.  Msaada huo ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani inayoadhimishwa Duniani kote Machi 8 ya kila mwaka.

Wanawake watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakiwa na Maafisa Magereza baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya  wafungwa, mahabusi wanawake na watoto wao katika Gereza Kuu Isanga jijini Dodoma.  Msaada huo ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani inayoadhimishwa Duniani kote Machi 8 ya kila mwaka.

                                                                  (Picha na NEC).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.