Habari za Punde

Ubunifu wa Mabadiliko ya Teknolojia Chachu Katika Kuleta Usawa wa Kijinsia

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akikabidhi majiko banifu 114 yanayotumia nishati safi na Salama ya kupikia katika hafla iliyofanyika Wilaya ya Bahi Kijiji cha Zanka  na Kigwe wamenufaika. Majiko hayo yametolewa na jumuiya ya wanawake ya wakala wa Nishati Vijijini ikiwa  ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya wanawake Duniani. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Godwin Gondwe.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi majiko banifu 114 yanayotumia nishati safi na Salama ya kupikia katika hafla iliyofanyika Wilaya ya Bahi Kijiji cha Zanka  na Kigwe wamenufaika. Majiko hayo yametolewa na jumuiya ya wanawake ya wakala wa Nishati Vijijini ikiwa  ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya wanawake Duniani. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Godwin Gondwe.

Sehemu ya wananchi wa Wilaya ya Bahi Kijiji cha Zanka  na Kigwe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (Hayupo pichani) katika halfa ya ugawaji Majiko banifu yametolewa na jumuiya ya wanawake ya wakala wa Nishati Vijijini ikiwa  ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya wanawake Duniani. 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki katika hafla ya ugawaji majiko Banifu 114 yanayotumia nishati safi na Salama ya kupikia katika hafla iliyofanyika Wilaya ya Bahi Kijiji cha Zanka  ambapo wananchi wa kijiji hicho na kijjii cha Kigwe wamenufaika. Majiko hayo yametolewa na jumuiya ya wanawake ya wakala wa Nishati Vijijini ambao ndio waandaaji wa tukio hilo ikiwa  ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya wanawake Duniani.

Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo, Senyamule amesema kuwa Matumizi ya kuni na Mkaa yamekuwa chanzo kikuu kinachotumika kwa kupikia hususani Maeneo ya Vijijini na kupelekea kutumika kwa kiwango kikubwa na hivyo kuleta athari katika mazingira.

“Serikali itaendelea kuweka vivutio kwa wazalishaji na wasambazaji wa Teknolojia na bidhaa za nishati safi na salama ya kupikia na kuongeza wigo wa upatikanaji wa bidhaa pamoja na kutoa unafuu wa gharama ili kuwezesha watumiaji kutumia bidhaa hiyo” Alisisitiza Mhe. Senyamule.

Zaidi ya tani milioni mbili za Mkaa zimekuwa zikitumika kwa mwaka kama nishati ya kupikia hivyo imeleta athari za mazingira na afya katika jamii, zaidi ya asilimia 85 ya kaya hapa nchini hutumia kuni na Mkaa kama chanzo kikuu cha nishati ya kupikia.

Naye Mkurugenzi Uendelezaji Masoko na Teknolojia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Bi. Advera Mwijage amesema jiko linatumia nishati mbili ambayo ni jiko la kuni na mkaa ambalo linaweza kutumika sehemu yoyote na inamsaidia mwananchi au mama wa kitanzania kupunguza gharama ya matumizi ya fedha na kupunguza ukataji wa miti ovyo.

Vilevile wenyekiti wa kijiji cha Kigwe Jeremia E.Sobayi amesema kila mwananchi  anatakiwa kuwa balozi mzuri  katika matumizi  sahihi ya majiko hayo na kila mmoja wao awe mlinzi wa mwenzake ili isije kutokea mtu akafanyia matumizi mengine nje ya malengo yaliyowekwa ya kutunza mazingira kwa kutokukata miti hovyo.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.