Mkoa wa
Kaskazini Pemba.
Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba uharibifu
wa mazingira ni changamoto kubwa ya nchi
na dunia kwa jumla, lakini athari zake kubwa zinabebwa nchi masikini ikiwemo
Zanzibar.
Mhe. Othman
ameyasema hayo kwa nyakati tofauti huko Wete na Micheweni Mkoa Kaskazini Pemba,
alipozungunza na watendaji na wafanyakazi wa Halmashauri ya Micheweni na wa
Baraza la Mji wa wete na Masheha katika ziara yake ya kuelezea mpango wa
serikali wa kuirejesha na kurithisha
Zanzibar kuwa ya kijani.
Amesema
kwamba hivi sasa maji ya bahari yamekuwa yakiingia katika arthi kavu na kuathiri
shughuli za kilimo na nyenginezo za kibinaadamu kwa sababu kina ya bahari
kimekuwa kikipanda kwa kasi sehemu mbali mbali duniani kutokana na changamoto
kubwa ya uharibu wa mazingira na ongezeko la joto.
Aidha Mhe.
Othman amesema kwamba nchi za Visiwa kama Zanzibar na maeneo yaliyozungukwa na bahari ndio waathirika
wakubwa wa tatizo hilo kutokana na kuyeyuka kwa theluji duniani baada ya kupanda kima cha joto sehemu
mbali mbali za duani.
Mhe. Makamu
amesema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa makusudi imeamua kuja na mpango wa
kukabiliana na hali ya uharibifu wa mazingira na kuirejesha Zanzibar kuwa ya
kijani ambao ni mkakati shirikishi wa Serikali na wananchi, viongozi na taasisi mbali mbali ili kujenga
utamaduni mpya wa kuwarithisha vijana kupenda kupanda miti na kuihifadhi.
Amesema
kwamba serikali inaelekeza juhudi kubwa katika
mpango huo kwa wananchi kwa vile wao ndio wenye dhamana ya kutengeneza
mwelekeo mpya utakaosaidia kuendeleza juhudi za utamaduni kwa wananchi wa kupanda
miti pamoja na kuwarithisha vijana utamaduni huo ili kulinusuru taifa na janga
la kimazingira.
Aidha
amesema kwamba hatua hiyo pia inakusudia kuwajengea utamaduni wananchi kuacha
kukata miti ovyo kwa matumizi ya shughuli mbali mbali ikiwemo za kilimo ili
kuepusha nchi kuwa na ukame na kukumbwa na tatizo la ukosefu wa huduma ya maji.
Amesema
kwamba hivi sasa kina cha maji kimepungua sana katika maeneo mbali mbali kama
vile za mabonde ya Zanzibar yaliyokuwa na kiasi kikubwa cha maji ya kutosheleza
mahitaji kutokana na kuwepo kasi kubwa ya mabadiliko ya
tabia nchi na binaadamu.
Amesema
kwamba maeneo mengi yaliyokuwa na mito mikubwa na maji ya kutosha hivi sasa yamekauka
kabisa jambo ambalo limechangia kuepo uhaba wa maji kwa kuwa hata hayo
yanayopatikana yanalazimika kutafutwa katika visima vya kina kirefu.
Ameongeza
kwamba ni lazima wananchi kuwa na
utamaduni mpya wa kuacha kuyageuza majangwa maeneo ya mapori kwa kuikata miti
ovyo na badala yake waendeleze juhudi za kupanda miti kwa kuanza hatua za
kupanda miti kwenye nyumba zakuishi.
Aidha
amewakumbusha wananchi kwamba miti ni uchumi mkubwa iwapo juhudi zitafanyika
kwa kuwa miti mingi inayopandwa katika kipindi kifupi inaweza kuuzwa kwa
thamani kubwa kutokana na mahitaji yanavyongezeka siku hadi siku.
Naye Kaimu
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba
Ndugu Matar Zahor Masoud, amesema kwamba ni vyema wananchi wakajiweka tayari
katika kutekeleza mpango huo utakapoanza kwa kuwa ni jambo muhimu litakaloinusuru
nchi isiharibike zaidi kimazingira.
Amefahamisha
kwamba katika kufanikisha mpango huo ni busara jamii ikatanabahi kwa kuwaanda
watoto katika utamaduni mpya wa kuanzisha utaratibu wa kupanda na kuhifadhi
miti tangu wakiwa skuli katika hatua za awali hadi wanapomalizia ili wazoee na
kukua na utamaduni huo.
Mwisho.
Imetolewa
na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha
habari leo tarehe 07.03.2023.
No comments:
Post a Comment