Habari za Punde

Dua ya Kumuombea Mwanamapinduzi Marehemu Hafidh Suleiman Almasi

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Jamal Kassim Ali akijumuika na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali pamoja na wanafamilia katika Dua ya kumuombea Mhe,Hafidh Suleiman Almasi Ikiwa ni muendelezo wa Maadhimisho ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar hafla iliofanyika Kijijini kwao Kinduni Kichungwani kaskazini Unguja.

Baadhi ya Wananchi mbalimbali waliohudhuria katika hafla ya kumuombea Dua Mhe,Hafidh Suleiman Almasi Ikiwa ni muendelezo wa Maadhimisho ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa ,Waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar hafla iliofanyika Kijijini kwao Kinduni Kichungwani kaskazini Unguja.








Na Khadija Khamis Maelezo Zanzibar 05/04/2023

https://mail.google.com/mail/u/0/images/cleardot.gif

Waziri wa Nchi,  Afisi ya Rais, Ikulu Mheshimiwa Jamal Kassim Ali amesema mchango  wa Viongozi Waandamizi  waliyojitoa muhanga kugombania nchi ili kuhakikisha uhuru unapatikana iko haja ya kuwaenzi na kuwakumbuka kutokana na juhudi walizozifanya.

 

Hayo ameyasema huko Kinduni Kichukwani, Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja wakati wa hafla ya  kufanya ziara na kusoma dua katika Kaburi la  Marehemu Hafidhi Suleiman Almas

 

Amesema viongozi hao wametoa mchango mkubwa katika kupambana na kugombania uhuru wa taifa lao kwa hali na mali hadi kufikia kujivunia matunda na maendeleo nchini.

 

Ameeleza kuwa viongozi hao  waliotangulia mbele ya haki wameweka historia nzuri isiyosahaulika  nchini na kuacha kumbukumbu kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

 

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahamud amesema Shughuli hiyo ya ziara na Kisomo cha dua imeasisiwa mwaka jana kwa hapa Zanzibar  mwanzo kulikuwa na Siku ya Mashujaa ya kuwaenzi na kuwakumbuka viongozi wa kitaifa.

 

“Ni dhahiri kwamba nia ya Serikali ni njema  ya kutoa dua kwa viongozi wa kitaifa ya kuwaenzi waasisi hao  hivyo iko haja ya kuwaombea dua” alifahamisha Mkuu wa Mkoa huyo.

 

Kwa upande wa Kiongozi wa Familia Iddi Hafidh Suleiman (Sancho) amewashukuru viongozi waliopanga mpango huo wa dua kwa Marehemu pamoja na walioshirikiana kufanikisha hafla hiyo

 

Ameomba kuwepo na mashirikiano ya pamoja  kwa familia  na wajane wa Marehemu hao ambao walijitoa muhanga kuhakikisha wanapata uhuru wa nchi yao

 

Dua hiyo imeongozwa na Sheikh Suleiman Simai Ali kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar kwa kushirikiana na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali  pamoja na  wanafamilia ,

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.