Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Amekutana na Kuzungumza na Balozi wa Ubelgiji Ikulu Zanzibar

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Balozi wa Ubelgiji Nchini Tanzania Mhe Peter Huyghebaert, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Ubelgiji Nchini Tanzania Mhe. Peter Huyghebaert, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Balozi wa Ubelgiji Nchini Tanzania Mhe. Peter Huyghebaert, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imejikiza zaidi kwenye teknolojia ya kisasa ili kuboresha sekta ya utalii kwa kuimarisha miundominu ya kisasa ya utoaji huduma bora kupitia viwanja vya ndege vya Zanzibar ili kuwavutia watalii wengi zaidi kutoka mataifa mbambali ya dunia wanaoitembelea Zanzibar ili wakirudi kwao wawe mabalozi wazuri wakusimulia mazuri yanayopatikana kwenye visiwa vya Unguja na Pemba na Tanzaia kwa ujumla.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Mhe. Peter Huyghebaert, Ikulu Zanzibar aliefika kujitambulisha.

Dk. Mwinyi, alimueleza balozi huyo kwamba Zanzibar utalii ndio sekta mama ya uchumi ambao inahusisha na sekta nyengine za uwekezaji kupitia sera yake ya uchumi wa Buluu.

Rais Mwinyi alisema Uhusiano uliopo baina ya Ubelgiji na Tanzania ikiwemo Zanzibar kumekuwa na urafiki mzuri baina yao kwani nchi imekuwa ikipokea watalii wengi kutoka huko.

Alisema kupitia sekta ya utalii kumekuwa na safari za ndege za moja kwa moja kutoka Ubelgiji hadi Zanzibar na kumueleza balozi huyo uhusiano uliopo baina ya pande mbili hizo anaamini wataalii zaidi wataongezeka katika kuimarisha urafiki wao.

“Zanzibar tuna safari za ndege za moja kwa moja kutoka Ubegiji, hali hii pia imeongeza watalii wengi kutoka huko, tunaamini idadi itaongezeka zaidi kutokana uhusiano mzuri baina yetu” alisifu, Dk. Mwinyi.

Akizungumzia sekta ya Afya Rais Dk. aliueleza balozi huyo kuangalia uwezekano wakuimarisha ushirikiano zaidi kwenye sekta hiyo hasa masuala ya TEHAMA ambako eneo hilo lina uhitaji zaidi ili kuongeza ujuzi na kubadilishana uzoefu kwa wafanyakazi na wahudumu wa fani hiyo kupitia taasisi ya Karume amako vijana wengi  huchukua fani ya Afya.

Pia Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi Huyghebaert ikiwa Ubelgiji ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) yenye miradi mingi ya maendeleo kuangalia zaidi fursa zilizopo kupitia ushirikiano wa diplomasia uliopo baina ya Ubelgiji na Tanzania ikiwemo Zanzibar kunufaika na fursa zilizopo huko na uwezekano wa kuzifikia katika kuimarisha zaidi uhusino baina yao.

Kwa upande wake Bolozi Peter Huyghebaert, aliishurkuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kumpongera Rais Dk. Mwinyi kwa juhudi zake za kuiletea maendeleo Zanzibar.

Alisema urafiki wa diplomasia uliopo baina ya Ubelgiji na Tanzania ikiwemo Zanzibar anaamini utaendelea kuzaa matunda mazuri yatakayowanufaisha wananchi wa pande mbili hizo.

Alisema Ubelgiji imekua ikishirikiana zaidi na Afika kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo kwa sekta zote za taasisi za umma na binafsi.

Alimueleza Rais Dk. Mwinyi kwamba hadi sasa Ubelgiji inaendeleza miradi mbalimbali kwenye kanda tano za Afrika, Tanznia ikiwa miongoni mwao kwa kuyafikia maeneo mengi hasa kwenye sekta mtandao ikiwemo kushirikina katika masuala ya Afya mtandao ambako Ubekgiji na Tanzania wanashirikiana kwenye matumizi ya teknolojia ya kisasa kuangalia uwezekano wa kunusuru vifo vya watoto kabla ya kuzaliwa, aidha, masuala ya huduma za pasi mtandao ambako Ubelgiji inashirikiana na Idara ya uhamiaji na sekta nyengine kwenye ustawi wa maendeleo ukiwemo mradi wa “wanawake wanaweza” katika kuwainua wanawake kuendana na maadiliko chanya ya maendeo na kujikwamua kiuchumi kupitia taasisi za serikali na asasi za kiraia.

Pia balozi huyo alimuahidi Dk. Mwinyi kushirikiana kwenye maeneo mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuimarisha matumizi ya IT na teknolojia hasa kwenye sekta ya afya kwa kuimarisha huduma za Afya mtandao pamoja na kuangalia fursa zilizopo kupitia uchumi wa buluu jinsi ya kuwanufaisha wananchi wa pande mbili hizo katika kuendeleza uhusiano wa kirafiki uliopo baina yao.

Tanzania na Ubelgiji zimekua na uhusiano wa diplomasia na biashara  tangu miaka ya 1980 ambapo kwa mara ya kwanza Ubelgiji ilifungua ubalozi wake Dar es Salaam mwaka huo na Tanzania ilifungua ubalozi wake mji mkuu wa nchi hiyo, Brussels ambako balozi wa Tanzania nchini humo ni Mhe. Jestas Abouk Nyamanga tangu mwaka 2019

IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.