Habari za Punde

Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar aongoza kikao kazi na watendaji wakuu wa ofisi yake

MAKAMU wa kwanza wa rais wa Zanzibar (KUSHOTO) akiwa katika kikao kazi na watendaji wakuu wa ofisi yake leo tarehe 31.07.23. kushoto  ni ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk Omar Dad Shajak . Picha na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais.

MAKAMU wa kwanza wa Rais wa Zanzibar (katikati shati nyeupe) akiwa katika kikao kazi na watendaji wakuu wa ofisi yake leo tarehe 31.07.23. kulia ni waziri wan chi ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Mhe, Hasrous Said Suleiman  na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk Omar Dad Shajak na kushoto kwa katibu ni Mkurugenzi wa Mipango sera na Utafiti Nd. Daima Mohammed Mkalimoto.

 Picha na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais.


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka watendaji mbali mbali katika taasisi na Idara za serikali nchini kuzingatia na kufuata vilivyo sera  za Idara zao kwakuwa ndio zenye miongozo muhimu  katika kufanikisha utekelezaji wa malengo  waliyopangiwa.

Mhe. Othman ameyasema hayo alipokutana na watendaji wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi yake katika kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa malengo na mipango  mbali mbali waliyojiwekea  ndani ya wizara hiyo sambamba na kufahamu changamoto walizonazo na kutafuta njia bora ya  pamoja kuzitatua.

Mhe. Othman amesema kwamba sera zinapofuatwa na kusimamiwa vyema  zinaweza kurahisisha utekelezaji  wa mipango iliyopo na ijayo  kwa mambo mbali mbali mbali na hivyo kuongeza ufanisi na mafanikio kazini.

Amewataka watendaji hao kuzidisha mashirikiano na watendaji mbali mbali wanaowasimami na kwamba kuhakikisha wanawapongeza pale wanapofanya vyema katika utekekezaji wa majukumu yao lakini na kuwaelekeza pale wanapoonekana kutotimiza wajibu wao ipasavyo.

Amefahamisha kwamba zipo baadhi ya taasisi  serikalini wanapopanga na kutekeleza mipango mbali mbali hawazingatii sera za taasisi zao  jambo ambalo ni nikinyume na utungwaji wa sera hizo ambapo zinapofatwa hurahisisha mambo mengi ya kiutendaji.

Aidha, Mhe. Othman amewataka watendaji hauo kusimaia na kufuata kwa makini taratibu na sheria za fedha kwa kuwa jambo hilo linapotokea huwa linaharibu taswira ya ofisi na kiongozi anayesimamia taasisi hiyo.

Akizingunzia suala la mapambano dhidi ya dawa za kulevya, Mhe. Othman amesema kwamba suala hilo bado ni gumu kiutekelezaji na kwamba ni muhimu kwa jamii na viongozi kubadilika na kulichukulia suala hilo kwamba ni la kitaifa badala ya kuliona kwamba ni la mamlaka inayohusika na mapambano dhidi ya dawa za kulevya poekee.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi wa Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe. Harous Said Suleiman amesema kwamba kuna umuhimu wa kuwepo mkakati wa kutolewa elimu kwa umma kwa masuala mbali mbali yanayotekelezwa na taasisi na idara mbali ,mbali ili jamii iweze kufahamu mambo yanayotekelezwa na serikali.

Kwa upande wake Kamshina Mkuu wa Mamlaka ya  kupambana na kudhibiti dawa za Kulevya Kanal Burhan Nassor amesema kwamba Mapambano dhidi ya dawa za kulevya Bado ni changamoto kubwa kulingana na ukubwa wa tatizo lilivyo kwa kuwa bado madawa ya kulevya yanaendelea kuingia Zanzibar kupitia njia mbali mbali.

Hata hivyo amesema kwamba suala hilo pia linaendelea kuwa gumu kutokana na kukosa mashirikiano kutoka kwa baadhi ya watendaji  katika taasisi mbali mbali za ulinzi na usalama jambo ambalo linadhoofisha juhudi za mapambano hayo.

Aidha amesema kwamba kutokana na hali hiyo ufanisi  katika mapambanoya Dawa za kulevya Zanzibar unaendelea  kuwa changamoto na kuwa na mafanikio madogo na kwamba kesi nyingi zimekuwa zikikosa ushahidi mahakamani na watuhgumiwa kuachiwa huru .

Amesema Mamlaka hiyo imefungua jumla ya kesi 449  Unguja na Pemba  ambapo zipo katika hatua mbali mbali za kisheria ambapo kati ya hizo 70 zipo katika hatua ya upelelezi, kesi 19 zipo kwa mkemia Mkuu na 13 zipo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka wakati kesi 36 zimefungwa na  kesi 311.

Amesema katika ya kesi 311 zilizofikishwa mahakamani kesi 187 zinaendelea, kesi 107 zimeachiwa huru na kesi  19 tu ndio washitakiwa wametiwa hatiani kutokana na changamogto ya kukosa ushiorikiano kutokahata kwa baadhi ya mahakimu na mashahidi huru ambao baadhi hupatiwa vitisho kutoka kwa watuhumiwa.

Amesema kwamba mamlaka hiyo inakusudia kuifanyia marekebisho sheria ya mamlaka hiyo ili kutoia uwezo zaidi wa kuendeleza mapamnbao hayo  na kuondosha tatizo la madawa ya kulevya hapa Zanzibar .

Mwisho

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar

31, Julai 2023.    

 

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.