Na.Mwandishi Wetu Havana,CUBA.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiambatana na Mama Mariam Mwinyi pamoja na ujumbe wake amewasili Havana, Cuba kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa kundi la 77 na China.
Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jose Marti Rais Dk. Alipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe.Balozi Humphrey Herson Polepole na maafisa wengine wa Ubalozi wa Tanzania na Cuba.
Ushiriki wake katika Mkutano huo ambao unatarajiwa kufunguliwa tarehe 15 Septemba,Rais Dk.Hussein Ali Mwinyi anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.
Baadae Rais Dk. Mwinyi atafungua rasmi Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Cuba.
No comments:
Post a Comment