Mhe. Hemed ambae ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Tanga ameyasema hayo kwa nyakati tofauti alipokuwa akizungumza na Viongozi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Lushoto na Wilaya ya Korogwe akiendelea na ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Tanga.
Amesema kuimarika kwa CCM Mkoani Tanga kunatokana na Miongozo inayotolewa na Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samua Suluhu Hassan anayoitoa kwa Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi.
Amesema ana Imani Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga kitashinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 hatua ambayo itatoa matumaini makubwa kushinda Uchaguzi Mkuu wa Dola ifikapo 2025.
Amefarijika kuona ziara za Viongozi wa Mkoa na Wilaya zinafanyika mara kwa mara pamoja Vikao vya Kikatiba na kuwataka Viongozi kushuka kwa wanaowaongoza ili kujua changamoto zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi hatua itakayoongeza Imani ya wananchi kwa CCM na Serikali yao.
Mhe. Hemed ambae ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali imesogeza miradi mingi ya maendeleo kwa wananchi wake ili kupata huduma bila ya kujali itikadi za wananchi.
Aidha amefahamisha kuwa Serikali itaendelea kuulinda na kuudumisha Muungano ambapo ndani ya muda mchache tayari hoja kadhaa za Muungano zimeshapatiwa ufumbuzi na siku chache zijazo Kamati inakwenda kumaliza hoja zilizobakia ili wananchi waendelee kunufaika na uwepo wa Muungano huo.
Nae Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga na Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Mkoa huo Ndg. Al - Shaymaa John Kwegyir ameeleza kuwa UWT inaendelea na ziara za mara kwa mara kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025 pamoja na kuhubiri mambo mazuri yaliyofanywa na Serikali katika Mkoa huo.
Aidha amesema wameweza kuwafikia wazazi na walezi na Kushajihisha kusimamia malezi mazuri kwa watoto ili kumaliza janga la mpromoko wa maadili ambalo humaliza nguvu kazi ya Taifa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Lushoto Ndg Ali Salum Dafa ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Lushoto kimeendelea kuimarisha Chama kwa ziara za mara kwa mara, kukaa vikao vya kikatiba pamoja na kuboresha Miradi ya Chama hatua ambayo inadhihirisha ushindi wa CCM katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na Uchaguzi wa Dola mwaka 2025.
Amesema maendeleo yanayoendelea kupatikana Mkoa wa Tanga yanatokana na mashirikiano yaliyopo baina ya Uongozi wa CCM Mkoa wa Tanga na Wilaya zote pamoja na Serikali ya Mkoa na za Wilaya kuamua kufanya majukumu yao kwa pamoja hatua ambayo inaongeza kasi ya uwajibika kwa watendaji wa Chama na Serikali katika kuwatumikia watanzania.
Abdulrahim Khamis
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
12 /10/ 2023
No comments:
Post a Comment