Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Atembelea Jumuiya ya ZABA Kitogani

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akipokea maelezo kutoka kwa naibu Katibu wa Jumuiya ya Wafugaji nyuki Zanzibar Nd. Abdu Baruan (kulia) huko Kitogani wilaya ya kusini Unguja. Mhe. Makamu alifanya ziara kuona shughuli za ufugaji nyuki huko kitogani leo tarehe 13.12.2023. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akipokea maelezo kutoka kwa  Katibu wa Jumuiya ya Wafugaji nyuki Zanzibar Nd. Khamis Ussi (aliyekaa) huko Kitogani wilaya ya kusini Unguja. Mhe. Makamu alifanya ziara kuona shughuli za ufugaji nyuki huko kitogani 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akipokea zawadi kutoka kwa  Hanna Schnnack wa Jumuiya ya Wafugaji nyuki Zanzibar (kulia) huko Kitogani wilaya ya kusini Unguja. Mhe. Makamu alifanya ziara kuona shughuli za ufugaji nyuki huko kitogani
 

Makamu Kitogani na ZABA                           13.12.20232

Mkoa wa Kusini Unguja

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba ufugaji wa nyuki ni miongoni mwa mazao yenye fursa kubwa kiuchumi kwa wananchi wanaojishughulisha na kazi hiyo jambo  litakalochangia  kukuza kipato chao na kuweza kupiga hatua katika kupambana na umasikini.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko Kitogani Mkoa wa Kusini Unguja alipotembelea Jumuiya ya Wafugaji Nyuki Zanzibar ( ZABA), ili kuona jitihada zinazofanywa na wanajumuiya hao katika kuendeleza kazi ya ufugaji nyuki.

Mhe. Makamu amesema kwamba kutokana na hali hiyo kuna haja ya suala hilo la ufugaji na uchakataji wa bidhaa za nyuki kulifanya kuwa ni jambo la kitaifa kutengenezewa mazingira yatakayoleta  faida zaidi kwa wananchi na taifa kwa jumla.

Hata hivyo,  Mhe. Makamu amesema kwamba suala la kuwepo sera na sheria makhusi ya mazao ya nyuki na uchakataji wake ni changamoto ambayo serikali inahitaji kuifanyia kazi ili kuliwekea mipango mizuri zaidi na kulifanya  suala hilo la mazao ya nyuki kuliongezea tija kwa wananchi na taifa kwa jumla.

Amesema kwamba kinachohitajika zaidi ni kujenga mazingira ya kuweza kuzalisha asali na mazao mengine yanayotokana na asali ili kuweza kuuza kwa bei kubwa kama zinavyofanya nchi nyengine mbali mbali duniani ambao wamefaidika sana na suala hilo.

Amesema kwamba serikali inahitaji kujenga uwelewa zaidi kwa wananchi na watendaji mbali mbali na kwa pamoja kulifanya zao hilo kwamba ni lakitaifa ambalo linahitaji kuendelezwa kwa juhudi za pamoja hasa katika uchakataji wa bidhaa za nyuki jambo litakalokuwa na manufaa makubwa na kueleta tija zaidi.

Ameongeza kwamba iwapo wafugaji wa nyuki wataweza kuzalisha kwa wingi na kwa ubora kuliko ilivyo sasa pamoja na kujitangaza ipasavyo katika masoko mbali mbali duniani zao hilo litaweza kuuzwa kwa thamani ya bei kubwa kama ilivyo kwa nchi nyengine  duniani ambapo bei ya asali ni kubwa na yenye manufaa sana kwa wafugaji .

Amesema kwamba Zanzibar inabahati ya kuwa asili ya kuwa na bidhaa zenye ubora sana na kwamba asali ya Zanzibar pia nimiongoni mwa zenye ubora na inayoweza kuuzwa kwa thaman kubwa iwapo itachakatwa kiutaalamu na kutangazwa zaidi katika masoko tafauti.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Ayoub Mohammed Mahamoud, amewahidi wanakikundi hao kwamba serikali ya mkoa huo itachangia gari nane za fusi kwa jumiuya hiyo ili waweze kutengeneza eneo la maegesho ya magari kwa wanaotembelea eneo hilo sambamba na kutoa pikipiki pamoja na kuchangia tangi la maji ili kuwanga mkono umoja huo wa wafugaji nyuki.

Amesema kwamba mkoa huo una misitu mikubwa ya kitaifa miwili na  jumla ya misitu ya jamii ipatayo 25 ambayo iwapo itatumika vyema  inaweza kuwa ghala kubwa la asali kwenye mkoa huo.

Mapema naibu Katibu wa Umoja huo Abdu Baruan Abdalla ameomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto mbali mbaki za ushirika huo ikiwa ni jitihada za kuboresha mazingira  ya ufugaji nyuki na uchakataji wa mazao yatokanayo na nyuki kuwa na faidia kwao na taifa kwa jumla.

 

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Disemaba 13, 2023

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.