Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba kujengwa kwa Barabara ya
Kipapo -Mgelema mkoa wa kusini Pemba kutasaidia kuondosha changamoto kubwa ya
tatizo la usafiri kwa wananchi wa maeneo hayo na kuwataka waitumie Zaidi kwa
manufaa ya kiuchumi .
Mhe. Othman ameyasema hayo
alipozungunza katika ufunguzi wa Barabara ya Kipapo- Mgelema wilaya ya Chake
chake Pemba ikiwa ni shamra shamra za
sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar kutimia miaka 60.
Amesema kutokana na juhudi za
serikali kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa awamu ya kwanza yenye urefu wa
kilomita 5.3 kutawawezesha wakulima kusafirisha mazao yao kwa urahisi na kuwepo unafuu wa gharama kwa wananchi wa
maeneo hayo.
Aidha amesema kwamba hatua hiyo pia
itawasaidia wananchi kuzifikia kwa wepesi huduma mbali mbali ikiwemo elimu na
Afya sambamba na unafuu wa usafiri wa abiria .
Mhe. Makamu amewataka wananchi wakaazi waliopitiwa na Barabara hiyo
kuhakikisha kwamba wanaitumia kwa maslahi ya kiuchumi ikiwa ili kusaidia kukuza
maendeleo yao hasa katika sekta za kilimo na biashara.
Sambamba na hayo Mhe. Othman
amewakumbusha wananchi hao kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti ya
uchumi na matunda pamoja na mengineyo kwa kuwa kufanya hivyo kutawasaidia
kiuchumi.
Mhe. Othman ameongeza kwamba
jitihada za ujenzi wa barabara pia
zitawawezesha wananchi kujishughulisha kwa wepesi na shughuli za biashara mbali
mbali na kuweza kupata kipato jambo litakalochangia kupunguza umasikini kwa
wananchi hao ikiwa ndio faida ya
Mapinduzi ya mwaka 1964.
Amefahamisha wananchi hao kwamba
ujenzi wa barabara unagharama kubwa ambapo kwa makisio ya chini kilomita moja
hujengwa kwa wastani wa dola laki sita za Marekani ambazo ni Zaidi ya shilingi
bilioni 1.3 za Tanzania .
Hivyo, amewataka wananchi
kuzithamni juhudi hizo za serikali kwa kila mmoja kutimiza wajibu katika
kuzitunza na pia kuzingatia matumizi sahihi ya barabara ili ziendelee kudumu na
kuwanufaisha Zaidi wananchi.
Kutokana na hatua hiyo
ameitaka wizara ya Ujenzi Mawasiliano na uchukuzi Zanzibar kuhakikisha
wanatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya barabara.
Amesema kwamba serikali kwa
kuwathamini wananchi wake tayari imetumia Zaidi ya shilingi milini mia tano na
sabiini na mbili kuwalipa fiadia wananchi ambao mashamba na nyumba na zao yao yameathirika kutokana na kupitia na
ujenzi wa barabara hiyo.
Akizungunzia
suala la janga la udhalilishaji Mhe. Othman amewataka wananchi wote kushiriki
katika mapambano hayo lakini pia kuacha tabia iliyozuka kwa baadhi ya watu
kulifanya suala la udhalilishaji kwamba ni biashara na kuwabambikizia kesi
wananchi wasiohusika na masuala hayo.
Naye Waziri wa Mawasiliano na
usafirishaji Zanzibar Dk. Khalid Salum Abdalla amesema amesema kwamba chachu ya
maendeleo ya kiuchumi ni kuwepo miundombinu bora ikiwemo ya barabara na viwanja
vya ndege na kwamba serikali ya mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikitilia maanani
sana suala hilo katika jitihada za kukuza uchumi na maendeleo kwa wananchi wa Unguja na Pemba.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba
Matar Zahor Masoud amesema kwamba ujenzi wa barabara hiyo ni hatua muhimu ya
wananchi wa eneo hilo kuwezeshwa kiuchumi na kwamba Zaidi ya nusu ya karafuu
zote zinazozalishwa Pemba zinatoka katika mkoa wa Kusini na eneo hilo likiwa
miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa zao la karafu.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo Bi Khadija Khamis Rajab
amesema kwamba barabara hiyo inauwezo wa kupita magari yenye uzito usiozidi
tani kumi na kwamba wananchi wote wanao wajibu wa kuhakikisha kwamba wanaitunza
barabara hiyo ili iweze kudumu .
Mwisho .
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 28.12.2023.
No comments:
Post a Comment