Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Amejumuika na Viongozi Mbalimbali Katika Viwanja vya Karinjee Kutoka Heshima za Mwisho kwa Marehemu Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Februari 13, 2024, amejumuika pamoja na Viongozi wa Serikali, Dini na Wanasiasa Mashuhuri, Viongozi Wastaafu, Mabalozi na Wanadiplomasia, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Familia na Wananchi, katika Hafla ya Kuuaga Mwili wa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.

Hafla hiyo ambayo imefanyika katika Viwanja vya Karimjee, imeongozwa na Mgeni Rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip  Mpango.

Katika hafla hiyo, Mheshimiwa Othman ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Februari 13, 2024.










Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Februari 13, 2024, amejumuika pamoja na Viongozi wa Serikali, Dini na Wanasiasa Mashuhuri, Viongozi Wastaafu, Mabalozi na Wanadiplomasia, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Familia na Wananchi, katika Hafla ya Kuuaga Mwili wa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.

Hafla hiyo ambayo imefanyika katika Viwanja vya Karimjee, imeongozwa na Mgeni Rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip  Mpango.

Katika hafla hiyo, Mheshimiwa Othman ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Februari 13, 2024.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.