Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Bw. Mohammed Kiande, akizungumza na Timu ya Wataalam ya kutoa Elimu ya Fedha, kutoka Wizara ya Fedha na Taasisi zake, walipofika Ofisini kwake kabla ya kuanza kutoa elimu ya fedha ikiwa ni mwendelezo wa zoezi la kutoa elimu hiyo kwa wananchi wa makundi mbalimbali katika Kata ya Nyigogo, Wilaya ya Magu, Mkoa wa Mwanza.

Baadhi ya wajasiriamali na wananchi kutoka Kata ya Shishani, Kisesa na Nyanguge Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza, wakiwa katika Ukumbi wa Halmashauri ya Magu pamoja na Timu ya Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha na Taasisi zake Wilayani humo, wakichangia mada mbalimbali kuhusu elimu ya fedha waliyoipata kupitia njia ya filamu yenye maudhui kuhusu matumizi sahihi ya fedha, umuhimu wa kupanga bajeti na kuitekeleza, umuhimu wa kusajili vikundi vya huduma ndogo za fedha , utunzaji wa fedha binafsi, umuhimu wa kushirikisha familia na watu wa karibu kwenye masuala ya fedha na uwekezaji, umuhimu wa kukata bima ya biashara na mali nyingine.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WF, Mwanza)
No comments:
Post a Comment