Habari za Punde

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Amefungua Kongamano la Cha cha Kisima cha Mafanikio

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  akitazama bidhaa mbalimbali alipotembelea banda la Maonesho la Baraza la Sanaa Taifa  (BASATA) kabla ya kufungua Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio kwenye Viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kisima cha Mafanikio, Esther Kimweri , wa pili kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania ( BASATA) , Dkt. Kedmon Mapana na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Sanaa za Maonyesho kutoka Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) Lilian Shayo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama bidhaa mbalimbali alipotembelea banda la maonesho la Masai Market Arusha lililo chini ya Baraza la Sanaa la Taifa  (BASATA)  kabla ya kufungua Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio lililofanyika kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025. Kushoto ni Flament Kivuyo na wa pili kushoto ni Sarah Robert  wote kutoka Masai Market  Arusha
Wazri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza  Zaituni Iddi  (kulia) ambaye ni mwanachuo wa fani ya Umeme wa Majumbani kutoka VETA Arusha,  alipotembelea banda la maonesho la VETA kabla ya kufungua Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025. Wa pili  kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Kisima cha Mafanikio, Esther Kimweri.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  na viongozi wengine wakiimba Wimbo wa Taifa wakati Waziri Mkuu alipofungua Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio  kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025.  Kulia kwake ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Chama cha Kisima cha Mafanikio, Esther Kimweri
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza alipofungua Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua nembo ya Chama cha Kisima cha Mafanikio baada ya kufungua Kongamano la chama hicho kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025.  Kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi  na  kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Kisima cha Mafanikio, Esther Kimweri.
Baadhi ya washiriki wa ufunguzi wa Kongamano la Chama cha Kisima cha Mafanikio wakimsikiliza mgeni rasmi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza kwenye viwanja vya Olasiti Garden jijini Arusha, Aprili 13, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.