Habari za Punde

Msajii wa Hazina Azungumza na Waandishi wa Habari Zanzibar

Mwenyekiti wa Zanzibar CEOs Forum Juma Burhan akizungumza katika Mkutano uliowajumuisha Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Na Sabiha Khamis   Maelezo 06.05.2025.

Ofisi ya Msajilli wa Hazina Zanzibar limeanzisha Jukwaa la kwanza la Wakuu wa Taasisi za Umma linalotarajiwa kuwa ni sehemu ya kujenga mshikamano kwa viongozi hao pamoja na kuimarisha utendaji unaolenga kuleta mafanikio ya kiuchumi na kijamii Zanzibar.

Akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari Msajili wa Hazina Zanzibar Waheed Ibrahim Mohamed Sanya huko Golden Tulip amesema Jukwaa hilo limetoakana na maono ya Ofisi hiyo pamoja na utekelezaji wa agizo la Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika Jukwaa la Wakuu wa Taasisi za Umma Tanzania Bara lililofanyika Zanzibar Januari, 2025.

Amesema kuwa wakuu wa taasisi za umma wana majukumu ya uwekezaji kwa umma katika kuendeleza ubora wa huduma, uvumbuzi wa kuongoza na kuchochea ukuaji endelevu wa kiuchumi.

“Mazingira ya kisasa ya kiuchumi na kiutendaji yanaendelea kwa kasi katika kufikia ubora wa shirika kunahitaji uongozi wenye maono na ushirikiano”, alisema Sanya.

Ameeleza kuwa Jukwaa hilo la kihistoria limelenga kuwakutanisha wakuu wa taasisi za umma na binafsi kutoka sekta mbalimbali ili kubadilishana mawazo, kujadili changamoto zinazofanana katika utekelezaji wa majukumu, kubadilishana uzoefu wa kiuongozi na kuanzisha mikakati ya pamoja ya kuboresha ufanisi na uwajibikaji katika taasisi hizo.

Msajili Sanya amefahamisha kuwa Jukwaa hilo litatumika kuwa ni msingi wa ushirikiano wa kimkakati, kukuza mazungumzo kwa kiwango kikubwa, kubadilishana maarifa, kutatua changamoto zilizopo, kufungua fursa na mitandao kati ya viongozi.

Nae Mwenyekiti wa Jukwaa la Wakuu wa Taasisi za Umma Zanzibar (Zanzibar CEOs Forum) Juma Burhan Mohamed amesema lengo kuu la Jukwaa hilo ni kufikisha huduma kwa wananchi, kutatua changamoto ambazo zinazikumba taasisi za umma pamoja na kutengeneza fursa kwa taasisi binafsi na wananchi kuweza kujua  na kukutana na wakuu wa taasisi za umma.      

Amesema kupitia Jukwaa hilo wataweza kuwaweka pamoja 

wakuu wa taasisi za umma ili kuwarahisishia wananchi 

kutatua changamoto zao na kujua fursa zinazopatikana kwa 

upande wa Serikali na sekta binafsi na kuzifahamu fursa hizo 

ambazo zitaweza kusaidia kwa lengo la kukuza uchumi wa 

Zanzibar.

Kwa upande wake CEO wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania 

Dkt. Said B. Kambi amesema kuwa Taasisi hiyo ipo tayari 

kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar ili 

kusaidia kuwajengea uwezo viongozi wa taasisi za umma na 

binafsi.


Jukwaa hilo la kwanza la Wakuu wa Taasisi za Umma 

litafanyika kwa muda siku 3 kuanzia 11 hadi 13, 2025 mgemi 

rasmi katikaJukwaa hilo anatarajiwa kuwa  Makamu wa Pili 

wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, kauli 

mbiu ni “Uongozi bunifu na Mashirikiano ni Muhimu ili 

kufikia Maendeleo Endelevu Zanzibar”. 

Msajili wa Hazina Zanzibar Waheed Muhammad Ibrahim Sanya akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

C,E,O wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania  Dk,Said Kambi akifafanua baadhi ya Maswali yalioulizwa na Waandishi wa Habari katika Mkutano kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Mratibu wa Zanzibar CEOs Forum Ahlaam Azzan akisoma Utambulisho wa Wafadhili katika Mkutano kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Mwandishi wa Habari wa ITV Farouk Kariym akiuliza Maswali katika Mkutano kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Mwandishi wa Habari muandamizi  Salum Vuai akiuliza Maswali katika Mkutano kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Baadhi ya Waandishi wa Habari pamoja na Wafanyakazi wa Zanzibar CEOs Forum waliohudhuria katika Mkutano kuhusiana na Jukwaa la Taasisi za Umma wenye lengo la kuleta Umoja ,Mshikamano na Ushirikiano,ambao unatarajiwa Kuanza Tarehe 11,12,13,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
 Picha na Yussuf  Simai -Maelezo  Zanzibar. 06/05/2025.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.