Habari za Punde

Waziri wa Fedha na Mipango Tanzaia Mhe.Dkt.Mwingulu Nchemba Akiwasilisha Bajeti ya Serekali ya Mwaka 2025/2026 Bungeni Jijiji Dodoma Juni 12,2025



 Wazirii wa Fedha , Dkt. Mwigulu Nchemba akionesha mkoba alipoingia bungeni jijini Dodoma kusoma Bajeti ya Seikali ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, bungeni jijini Dodoma, Juni 12, 2025
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba akisoma Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, bungeni jijini Dodoma Juni 12, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Na Saidina Msangi, WF, Dodoma
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), anamewasilisha Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali, ambapo ameliomba Bunge ridhaa ya kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 56.49 kwa Mwaka wa Fedha 2025/26.

Dkt. Nchemba ameomba ridhaa hiyo bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/26, ambapo bajeti  hiyo inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani ya shilingi trilioni 40.47, misaada shilingi trilioni 1.07 na mikopo ya shilingi trilioni 14.95.

‘‘Kati ya mapato ya ndani yanayotarajiwa, mapato ya kodi ni shilingi trilioni 32.31, mapato yasiyo ya kodi shilingi trilioni 6.48, na mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 1.68. Aidha, mikopo inajumuisha shilingi trilioni 6.27 kutoka vyanzo vya ndani na shilingi trilioni 8.68 kutoka vyanzo vya nje’’, alifafanua Mhe. Nchemba.

Alieleza kuwa makadirio ya matumizi ya Serikali ya shilingi trilioni 56.49 kwa mwaka 2025/26 yanajumuisha Stahiki za watumishi na michango ya pensheni (Serikali Kuu) shilingi trilioni 9.17 pamoja na  ununuzi wa bidhaa na huduma shilingi trilioni 5.58.

Aliongeza kuwa matumizi mengine ni malipo ya riba za mikopo shilingi trilioni 6.49; na ruzuku kwa taasisi za Serikali, mashirika ya umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 22.17 na shilingi trilioni 7.72 kugharamia malipo ya mtaji kwa deni la ndani na nje.

‘‘Katika Mwaka wa Fedha 2025/26 Serikali inatarajia kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 6.0 mwaka 2025 kutoka ukuaji wa asilimia 5.5 mwaka 2024, kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0 - 5.0 katika muda wa kati’’, alifafanua Mhe. Nchemba.

Aidha, Dkt. Nchemba alisema Serikali inatarajia kuongeza Mapato ya ndani kufikia asilimia 16.7 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 ikilinganishwa na asilimia 15.8 mwaka 2024/25 na mapato ya kodi kufikia asilimia 13.3 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 kutoka asilimia 12.8 mwaka 2024/25.

Dkt. Nchemba alisema vipaumbele vya bajeti ya mwaka 2025/26 ni pamoja na kuendelea kutekeleza na kukamilisha miradi ya kielelezo na ile ya kimkakati, kuimarisha sekta za uzalishaji zenye matokeo chanya katika kukuza uchumi, kuimarisha rasilimali watu hususan katika sekta za huduma za jamii na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili kuvutia ushiriki wa sekta binafsi katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

‘‘Maeneo mengine mahsusi ya vipaumbele ni pamoja na ugharamiaji wa Deni la Serikali; mishahara na stahiki za watumishi wa umma, pamoja na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027. Aidha, nipende kuwafahamisha Watanzania kuwa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 tutaugharamia kwa fedha zetu za ndani’’, alisema Mhe. Nchemba.

Aidha, Dkt. Nchemba alisema katika mwaka 2025/26, Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ukusanyaji wa mapato ikiwemo  kuendelea kuhamasisha umma kuhusu kutoa na kudai risiti za malipo za kielektroniki za EFD na kuboresha utaratibu wa ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vinavyosimamiwa na mamlaka za udhibiti.

‘‘Serikali itaendelea kuboresha Mfumo wa TAUSI ili kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vya Mamlaka za Serikali za Mitaa vinajumuishwa katika mfumo huo, kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya mashirika, taasisi za umma na wakala za Serikali ili kuhakikisha gawio na michango stahiki inawasilishwa kwa wakati na  kuendelea kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI)’’, alifafanua Mhe. Nchemba.

 

MABORESHO YA MIFUMO YA KODI.


Dkt. Nchemba alisema Serikali inalenga kufanya maboresho 


ya mfumo wa kodi, ikiwemo baadhi ya viwango vya kodi, tozo 


na ada zinazotozwa chini ya sheria mbalimbali pamoja na 


kuboresha taratibu za ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya 


Serikali ili kuwa na mfumo wa kodi ambao ni tulivu na wa 


kutabirika unaolenga  kuchochea shughuli mbalimbali za 


uzalishaji mali ndani ya nchi.


Mapendekezo ya kurekebisha mfumo wa kodi kwa mwaka 



2025/26 yanatarajiwa kuiongezea Serikali jumla ya shilingi 


milioni 4,260,023.77 ambapo baadhi ya mapendekezo hayo ni 


kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye viuatilifu 


vinavyotambulika kwa HS Codes 3808.61.00, 3808.62.00 na 


3808.69.00, ili kuwapa unafuu wakulima ya kupata dawa za 


kuua wadudu mashambani na hivyo kuongeza uzalishaji wa 


mazao nchini.

 

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye miamala ya 


ununuzi wa bima mtawanyo inayofanywa baina ya kampuni 


za bima na zile za bima mtawanyo ili kuongeza ushindani wa 


kampuni za ndani, kukuza Sekta ya Bima na kuhamasisha 


matumizi ya bima katika kukabiliana na majanga nchini.

 

Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 


0 kwenye bidhaa za nguo zinazotengenezwa kwa kutumia 


pamba inayolimwa nchini kwa kipindi cha mwaka mmoja ili 


kuleta unafuu kwa wakulima wa pamba na viwanda 


vinavyotengeneza nguo nchini.

 


Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 


0 kwenye mbolea inayozalishwa ndani ya nchi kwa kipindi cha 


miaka mitatu ili kuleta unafuu kwa wakulima na walaji hasa 


katika kipindi hiki ambacho dunia imetoka kwenye mdororo 


wa kiuchumi duniani.

 

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye mafuta ya 


kula yanayozalishwa ndani ya nchi kwa kutumia mbegu 


zinazozalishwa nchini kwa muda wa mwaka mmoja ili 


kuendelea kuleta unafuu wa bei ya mafuta ya kula nchini.

 

Kufuta Msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani unaotolewa 


kwenye ununuaji na uingizaji wa gaming supply. Hatua hii 


inalenga kuleta usawa katika utozaji wa kodi kwa kuwa 


michezo mingine kama vile mpira wa miguu ipo katika wigo 


wa utozaji wa kodi ya ongezeko la thamani. Hatua hii 


inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi 


milioni 322,022.5.

 

Kuweka sharti la msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani 


kwenye matairi ya trekta yanayotumika kwenye shughuli za 


kilimo yanayotambulika kwa HS Code 4011.70.00; dam liners 


zinazotambulika kwa Heading 39.20; forks (HS Code 


8201.90.00); reki (HS Code 8201.30.00); na shoka (HS Code 


8201.40.00) kutolewa baada ya kupata ridhaa ya Waziri 


mwenye dhamana ya masuala ya kilimo.

 

Kufuta msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye 


lami zinazotambulika kwa HS Code 2713.20.00 na 2715.00.00 


ili kuendana na azma ya Serikali ya kupunguza misamaha 


isiyo na tija ili kulinda mapato ya Serikali na kupunguza 


matumizi yanayohusiana na utoaji wa misamaha ya kodi. 


Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi 


cha shilingi milioni 85,606.2.

 

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye magazeti 


yanayozalishwa nchini pekee ili kupunguza gharama za 


magazeti hayo na hivyo kuwezesha upatikanaji wa taarifa 


muhimu. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali 


kwa kiasi cha shilingi milioni 1,274.4.

 

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye gesi asilia 


inayouzwa kwenda kwenye vituo vya kushindilia gesi kwa ajili 


ya matumizi ya magari ili kuweka unafuu kwa wawekezaji, 


kuvutia uwekezaji wa vituo vya kusambazia gesi asilia 


iliyosindikwa kwenye magari na kupunguza utegemezi wa 


mafuta na uzalishaji wa hewa ya ukaa.

 

Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye matanki na 


mitungi ya gesi ya kupikia zinazotambulika kwa HS Code 


7311.00.10 pamoja na mitambo ya kuondoa hewa ukaa yenye 


HS Code 8417.80.00 inayotumika katika uzalishaji wa mikaa 


mbadala. Hatua hii inalenga kupunguza gharama za 


upatikanaji wa bidhaa hizi ili kuhamasisha matumizi ya 


nishati safi ya kupikia nchini.

 

Kujumuisha masoko mtandao na huduma za masoko za 


kimtandao kwenye wigo wa tafsiri ya neno wakala wa huduma 


za kimtandao ili kutanua wigo wa kodi kwa kuweka ufafanuzi 


utakaopelekea kutatua changamoto zilizopo katika utozaji na 


usimamizi wa kodi ambapo tafsiri iliyopo sasa haijumuishi 


huduma hizo katika utozaji kodi. Hatua hii inatarajia 


kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 


116,073.4.

 

Kuweka unafuu wa kutoza kodi ya mapato kwa kundi la 


pikipiki ya miguu miwili, pikipiki ya miguu mitatu (Bajaji) na 


magari ya kubeba mizigo yenye uzito usiozidi Kilogramu 500 


ikiwemo Guta kwa kuweka utaratibu mpya wa kukadiria kodi 


ya mapato kwenye vyombo hivyo. Maboresho ya viwango vya 


kodi elekezi yanalenga kuweka unafuu wa kodi kwa kundi 


husika na hivyo kurahisisha utekelezaji wa sheria.

 

Kupunguza tozo ya ushuru wa huduma kutoka utaratibu wa 


sasa wa kutoza kiwango kisichozidi asilimia 0.3 ya pato ghafi 


kwenda kiwango mfuto cha asilimia 0.25 ya pato ghafi. Lengo 


la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na 


uwekezaji nchini pamoja na kuendana na masharti ya Mpango 


wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (MKUMBI).

 

Kupunguza kiwango cha ada ya ushuru wa hoteli (hotel levy) 


kutoka asilimia 10 hadi asilimia 2. Lengo la hatua hii ni 


kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini.

 

Kufuta ada za upakiaji (loading) na upakuaji (offloading) 


zinazotozwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinazohusiana 


na usafirishaji wa mizigo. Lengo la hatua hii ni kupunguza 


gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili 


kuendana na masharti ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya 


Biashara nchini (MKUMBI).

 

Kupunguza ada ya usajili wa pikipiki za biashara kutoka 


shilingi 340,000 hadi shilingi 170,000 kwa miaka mitatu 


ambapo ada husika italipwa wakati wa usajili wa awali pekee. 


Kupunguza ada ya leseni ya uendeshaji wa pikipiki, bajaji na 


guta kutoka shilingi 70,000 hadi shilingi 30,000.

 

KUGHARAMIA BIMA YA AFYA

 

Serikali inapendekeza kuanzisha vyanzo mbadala vya mapato 


ili kupunguza nakisi ya kibajeti kwa kufanya marekebisho

katika sheria mbalimbali. Aidha inapendekezwa asilimia 70 ya 


mapato yatakayoongezeka ipelekwe kwenye Mfuko wa 


Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (ATF) na asilimia 30 


ipelekwe kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote. 


Marekebisho hayo ni kama ifuatavyo:

 

Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 


147 ili kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vya kilevi 


vinavyozalishwa na vinavyoingizwa kutoka nje ya nchi kama 


ifuatavyo: shilingi 20 kwa bia zinazotambulika kwa Heading 


22.03; shilingi 30 kwa mvinyo unaotambulika kwa Heading 


22.04, 22.05, na 22.06; shilingi 50 kwa spirits na vinywaji 


vingine vinavyotambulika kwa Heading 22.08.

 

Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, 


SURA 147 ili kuongeza kiwango cha ushuru wa bidhaa kwenye 


huduma za mawasiliano ya kielektroniki kutoka asilimia 17 


hadi asilimia 17.5.

 

Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Barabara na 


Mafuta, SURA 220 ili kutoza kiasi cha shilingi 10 kwa kila lita 


ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa pamoja na 


kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, SURA 123 ili 


kutoza kiwango cha asilimia 0.1 kwenye thamani ya soko ya 


madini.

 

Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Michezo ya 


Kubahatisha, SURA 41 ili kuongeza kiwango cha kodi kwenye 


zawadi ya ushindi (Winning tax) kwenye michezo ya kubashiri 


matokeo (sports betting) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 15; 


na kwenye michezo ya kasino ya ardhini (land based casino) 


kutoka asilimia 12 hadi asilimia 15.

 

Kutoza magari na mashine (heavy machines) zinazoingizwa 


kutoka nje ya nchi kama ifuatavyo: Shilingi 50,000 kwa 


magari yenye ukubwa wa injini (CC) kati ya 0 -1000; Shilingi 


100,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 


1001-1500; Shilingi 150,000 kwa magari yenye ukubwa wa 


injini (CC) kuanzia 1501-2500; Shilingi 200,000 kwa magari 


yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 2501 na zaidi; Shilingi 


250,000 kwa mashine (Excavators, Bulldozers, Fork Lifts) 


zenye Heading 84.29 na 84.27.

 

Kutoza shilingi 500 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa 


huduma za usafirishaji kwa njia ya treni na kutoza shilingi 


1000 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za 


usafirishaji kwa njia ya anga. Hatua hizi kwa pamoja 


zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali  kwa shilingi milioni 


586,404.9.

 

KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA

 

Ili kuiwezesha nchi kuwa na sera bora za biashara na kuweka 


mazingira mazuri ya ufanyaji biashara baina ya wazawa na 


wageni, Serikali inatarajia kufanya marekebisho kwenye 


Sheria ya Utoaji wa Leseni za Biashara ikiwemo:

 

Kufuta kifungu cha 3(4) kinachozipa nguvu mamlaka za utoaji 


wa leseni za biashara kufunga biashara pale ambapo 


wafanyabiashara wamekiuka masharti ya Sheria husika. 


Lengo la hatua hii ni kuwaondolea kero wafanyabiashara na 


pia kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutofunga biashara.

 

Kuongeza kifungu cha 8(7) ambacho kinampa mamlaka 


Waziri mwenye dhamana na masuala ya biashara kuainisha 


shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa na 


wageni. 


Utaratibu wa utekelezaji wa kifungu hiki utafanywa kupitia 


Amri (Order) itakayotolewa na Waziri ambayo itakua na 


orodha ya shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa 


na wageni.

 

Dkt. Nchemba alisema bajeti hii inaendeleza na kukamilisha 


utekelezaji wa miradi, Kuchochea uchumi shindani na 


shirikishi, kuimarisha uzalishaji wa bidhaa viwandani na 


utoaji huduma, kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea 


maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu ili 


kuhakikisha ufikiwaji wa malengo ya Dira 2025.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.