Nikiwa
katika Daladala maeneo ya sogea nilikutana`na mkasa wa aina yake pale ambapo
kuna mtu alinadiwa mwizi na katika kusalimisha usalama wake aliona bora akimbilie
Msikitini na kujifungia ndani.
Nikiwasikiliza
abiria waliopo kwenye dala dala wakisimulia kisa na mkasa wa mwizi huyu na wengine ambao hutafuta himaya
ndani ya nyumba za ibada kulikuwa na riwaya tofauti za jinsi mwizi ambaye
pengine hata kusali hasali lakini mambo yanapomzidia anajua kwamba Waislamu wanaziheshimu
nyumba za Ibada na hivyo akiwepo humo basi yuko “salama” na maisha yake angalau
kwa muda mpaka wafike wanausalama kumshughulikia.
Msikiti ni
nyumba ya ibada kwa waumini wa dini ya kiislamu. Si ibada pekee inayofanyika
hapo bali pia ni nyumba ya utulivu, husomeshwa darsa na mafundisho ndani yake,
husaliwa, hufanywa dhikr na mengi mengineyo.
Ni nyumba
ambayo kila anaeingia ndani hupaswa kuwa katika hali ya utulivu bila ya
kushughulisha au kuwabughudhi wengine walio kwenye ibada tofauti sasa akiingia
mwizi katika hali hii sijui msikitini itakuwaje.
Tasawwar
Waislamu wanasali Jamaa Msikitini wakitekeleza Sala ya fardhi na ghafla mwizi
aingie humo kujisalimisha nafsi yake kukimbia kipigo ambacho laiti asingekimbilia Msikitini
kingeweza kusababisha mauti yake.
Je Waumini
Wanaosali unadhani watafanya kitu gani ilhali tayari wameghulishwa katika sala
zao?
tunavoambiwa tusiwache swala ya fardhi kwa kitu chochote
ReplyDelete