Na Masanja Mabula, PEMBA
JESHI la polisi mkoa wa Kaskazini Pemba limefanikiwa
kumkata mtu anayedaiwa kuwa ni mfanyabiashara maarufu wa bangi, Hamad
Hamad Bakari (70) mkaazi wa Jitenge shehia ya Mchangamdogo wilaya ya Wete.
Taarifa za jeshi hilo
zimeeleza kuwa wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiahsra huyo wa bangi akiwa na
mafurushi 74 yenye uzito wa zaidi ya kilo 14.
Mtuhumiwa huyo ambaye ni mlemavu alikamatwa jana majira ya
saa 4:30, asubuhi kufautia taarifa zilizotolewa na raia wema kwa jeshi la
polisi ambalo liliweka mtego uliofanikisha kumkata mfanyabiashara huyo.
Akithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Kamaishna Msaidizi Mwandaamizi Yahya Rashid Bugi, alisema alisema baada ya raia wema kutoa taarifa jeshi la polisi kwa kushirikiana na polisi jamii liliweka ulinzi na kufanikiwa kukamata majani hayo yakiwa kwenye mapolo.
“Tulipokea taarifa kutoka kwa wananchi ambao walidai
kuchoshwa na tabia ya mtuhumiwa ya kuendelea kuuza bangi, na alipokamatwa
alikiri kuwa bangi hiyo ni mali
yake na iliingia kisiwani hapa ikitokea Tanga kupitia bandaari ya mtambwe”,alisema
Bugi.
Alisema kuwa baada ya kukiri kuwa hiyo bangi ni mali yake, mtuhumiwa aliomba msamaha akiahidi
kutorejea tena kosa kama hilo,
jambo ambalo kamanda Bugi alipingana nalo na kwamba anatarajia kufikishwa
mahakamani kujibu shitaka linalomkabili.
Kutokana na kitendo hicho, Kamanda Bugi aliwataka wananchi hasa wanaoishi karibu na bandari kutoa ushirikiano na jeshi la polisi kuwafichua wanaoingiza dawa za kulevya ili kuwakinga vijana na wimbi la utumiaji wa dawa hizo.
Alisema wananchi wa Jitenge Mchangamdogo wamechoshwa na
vitendo hivyo na kuamua kuondoa muhali na kumfichua mfanyabiashara huyo.
"Lazima tuonde muhali tuwe tayari kuwahoji wananchi
wanaopita katika sehemeu zetu wakiwa na mizigo ambayo tuna itilia mashaka,
ambapo kwa kufanya hivyo tutaweza kudhibiti uingiazji na uuzaji wa dawa za
kulevya hpa nchini", Bugi.
Hata hivyo taarifa zilipatikana na Zanzibar Leo zinasema
kuwa mtuhumiwa aliwahi kukamatwa akiwa na majani makavu yanasadikiwa kuwa ni
bangi miaka kadhaa iliyopita ambapo aliahidi kutorejea biashara hiyo baada ya
kupelekwa mahakamani.
Aidha baadhi ya wananchi waliozungumza na mwandishi wa habari hizi walivitaka vyombo vinavyosimamia sheria kukunjuka na kutoa adhabu kali kwa wanaokamatwa na dawa za kulevya.
Aidha baadhi ya wananchi waliozungumza na mwandishi wa habari hizi walivitaka vyombo vinavyosimamia sheria kukunjuka na kutoa adhabu kali kwa wanaokamatwa na dawa za kulevya.
No comments:
Post a Comment