Wananchi mbali mbali wa vitongoji vya mji
wa Chcke chake, wakiangalia moto uliokuwa ukiounguza nyumba ya Riziki Hamad
Ali, huko Madungu chake chake jana ambapo nyumba hiyo iliteketea yote pamoja na
vitu vyote vilivyokuwemo ndani.(picha na Haji Nassor, Pemba )
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kikiwa katika
harakati za kuzima moto uliotokea jana kwenye nyumba ya Riziki Hamad Ali huko
Madungu Wilaya ya Chake chake Kisiwani Pemba, ambapo katika nyumba hiyo
kuliteketea kila kila kitu na hadi sasa chanzo cha moto huo hakijajulikana
(picha na Haji Nassor, Pemba)
Na Haji Nassor, Pemba
IKIWA majanga ya kuungua nyumba moto yakiendelea
kutikisa Kisiwa cha Pemba, jana tena kumetokezea moto mkubwa na kuunguza nyumba
yote na vitu vilivyokuwemo ndani ya nyumba hiyo huko Madungu Wilaya ya Chake
chake Mkoa wa Kusini Pemba
Kadhia hiyo
ilioanzia siku mbili kabla, kwa kuunguza kanga na begi kwenye nyumba za jirani
na kutoonekana kwa chanzo, jana ulianza majira ya saa 2:10 asubuhi, wakati
mwenye nyumba hiyo Riziki Hamad Ali akiwa anakwenda kazini.
‘’Bado hatujaelewa
chanzo cha moto huo mkubwa na sisi kama Jeshi
la Polisi tutafanya upelelezi wa haraka, lakini tunawapongeza KZU kwa kudhibiti
moto huo’’,alifafanua Kamanda huyo.
Mapema mmiliki wa
nyumba hiyo Riziki Hamad Ali (26), alisema kuwa aliondoka nyumbani kwake na
kwenda kazini ambapo kabla hajafika alipata taarifa ya kuungua nyumba yake
moto.
Akieleza kwa
masikikitiko alisema kuwa hakukua na kitu chochote cha matumizi ya ueme
kilichokuwa wazi na ameshangaa kupokea taarifa hiyo muda mfupi tu tokea
kuondoka.
Kwa kweli hadi
sasa sijaelewa chanzo cha moto huo maana nilipoondoka mimi kwenda kazini, vitu
vyote vimezimwa na wala vyengine havitumiki kabisa ’’,alieleza.
Baadhi ya
mashuhuda wa tukio hilo
walisema kuwa awali waliona moto mkubwa kutoka katika nyumba hiyo ambayo ilikuwa imekomewa na kupiga kelele na
wakaanza kuzima.
Walieleza kuwa baada
ya kuona hivyo baadhi yao
waliwapigia Kikosi cha Zimamoto na Uokozi na ghafla walifika na kuanza kuuzima
licha vitu vyote kuungua.
Taarifa
zilizopatikana katika eneo hilo
zilieleza kuwa siku mbili kabla ya kutokezea hayo, nyumba ya ndugu yake Riziki,
Ali Hamad kuliungua kanga moto na hapakuwa na chanzo jambo ambalo liliwashangaaza
waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo.
Tukio jengine la
maajabu lilitokezea kwenye nyumba hiyo hiyo ya Ali, mara hii kukiungua nguo
zilizokuwemo kwenye beki ambapo beki lilibaki salama na nguo zote kuteketea.
Hii inaifanya kuwa
nyumba ya 14 kukumbwa na ajali ya kuungua moto katika kipindi kisichozidi mwezi
mmoja Kisiwani Pemba, ambapo baadhi ya wananchi wanahusisha moto huo na iamani
za kishirikina.
Wiki iliopita
jumla ya nyumba 13 ziliungua moto kwa siku tofauti huko Tumbe Kaliwa Mkoa wa
Kaskazini Pemba , kwa maajabu kutokana na
kuunguza baadhi ya vitu na vyengine kubaki salama.
No comments:
Post a Comment