Habari za Punde

Wazanzibari Canada washerehekea Iydul Adh-ha

 
 
Wazanzibari kadhaa wakiongozwa na Jumuia ya wazanzibari nchini Canada, walimu na wazee wa madrasat al-ameen na kikundi cha darsa za wanawake cha wazanzibari cha al-hidayah, jana jumamosi oktoba 27, 2012, walijumuika pamoja katika kuadhimisha eid al-adh-ha katika ukumbi wa Lawrence Heights Community centre katika jimbo la north york, Ontario.

Katika hafla hiyo, kulitolewa mawaidha mbali mbali kama vile mmoja wa wazee wa watoto wa kizanzibari alipowasihi wazee wenzake kuwa waumini wa kweli na kuzingatia mafundisho ya dini yetu ya kiislamu kwa kuwafundisha watoto waishio katika nchi za kigeni maadili ya dini yao. alisistiza kwamba kuwa na imani siyo kujiita muislamu tu bali ni kutekeleza yake aliyotulea Allaah kupitia kwa mMume wake mpenzi Muhammad saw.

Naye Ustadhi Dullah wa Madrasat al-Ameen aliwasihi watoto ambao walikuwapo kwa wingi katika sherehe hiyo, kuwasikiliza wazee wao kwa kila la kheri wanalowambiwa na wache tabia ya kuguna wanapokatazwa jambo ambalo wao wanaliona ni zuri, lakini mzee wake anafahamu tosha kuwa halina manufaa kwao.

Alisisitiza kuwa watoto wajishughulishe zaidi na kuwaiga wazee wao katika kutekeleza nguzo za kiislamu kama vile kusali, kwenda misikitini siku za ijumaa wanapokuwa nyumbani, na kufanya ibada nyengine ambazo ndizo zitakazowasaidia siku ya hesabu mbele ya allaah. pia aliwataka wazee waache tabia ya kusema kuwa mtoto amemshinda hasiki anayoambiwa na badala yake atumia njia za busara kumfahamisha na kumuelekeza maadili yanayohusiana na silka za dini yetu na kizanzibari.

Naye Sheikh Abdulafatah amewashauri wazee wazee kufanya yake yaliyoelezwa na ustadh dullah ya kuwafundisha watoto wao yaliyo mema na kuwasisitiza kusoma qurani zaidi.

Alisema kwamba wazee watakutana kuandaa mikakati ya kuwaelimisha watoto wetu mambo yanayohusu itikadi zetu za kidini na kizanzibari na kuwakabidhi watoto hao wakiwa tayari kushika hatamu hizo na baadaye waje wawachie wenzao wao watakapokuwa njia kurejea kwa Allaah.

Aliendelea kusema kuwa mikusanyiko ya wazanzibari imepungua siku hizi kitu ambacho hakipendezi na itakuwa vizuri kama jambo hili litaendelezwa ili wazee waweze kuwapa maarifa watoto wao na kuwazoesha kukaa pamoja na kujuana.

Naye Ustadh Khalfan, ambaye ni Mwalimu Mkuu wa al-ameen, alimtaka mmoja wa wanafunzi wake wahitimu, ambaye sasa hivi ni mwanafunzi wa chuo kikuu na president wa wanafunzi wa chuo hicho, kuwaelimisha watoto wenzake faida za elimu. Abdallah Albaalawy, aliwataka watoto hao kujishughulisha zaidi na elimu na waache kupoteza wakati wao katika game za computer.

Pia aliwataka watoto hao kutokujishughulisha na masuala ya mtandao kama vile facebook na game na badala yake waitumie computer kwa kazi zao za skuli na kujielimisha mambo ambayo hawayajui ili kupanua akili zao. Aliwataka wafanye home work zao kwa wakati na pia wajishughulishe na michezo zaidi kuliko kujikandamiza katika kusikiliza miziki ya magharibi na mitandao isyowasaidia katika mustakabali wao

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wazanzibari kadhaa kutoka maeneo ya gta Toronto ambao kwa pamoja walifurahi kukutana baada ya muda mrefu kutawanyika. hata hivyo, baadhi ya wazanzibari walilazimika kuondoka kwa muda kwenda hospitali kuwawakilisha wenzao kumpa pole mama yetu mmoja ambaye alilazwa huko na kumuombea dua ya shifaa.

Hafla hiyo ilianza kwenye milango ya saa tisa jioni na kumalizika mnamo saa moja za jioni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.