Habari za Punde

Tuwe Pamoja kufunga Taasu’a na ‘Aashuuraa



Siku  -  Ijumaa na Jumamosi

Tarehe – 09- 10 Muharram 1434 (23-24 November 2012)

Unachotakiwa – Kufunga siku hizi mbili funga ya Taasu’a na ‘Aashuuraa      (tarehe 9-10 Muharram)

Kwa nini ufunge? – Kwasababu Mtume Muhammad Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam alifunga na alituamrisha waislamu tufunge.

Kwa nini Taasu’a na ‘Aashuraa? – Kwasababu Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam amesema kama “Nikijaaliwa kuwa hai mwakani nitafunga na Taasua ili kutofautiana na Mayahudi” (Muslim). Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam hakuwahi kufika mwaka uliofuatia.

Kwa tukio gani? Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam alipohamia Madina aliwaona Mayahudi waliokuwa wakiishi Madina (wakati huo) wakifunga siku hii na akauliza kwanini? Akaambiwa hii ni siku muhimu kwetu, ni siku adhimu siku ambayo Allaah Subhaanahu Wata’ala alimwokoa Nabii Musa ‘Alayhis Salaam kutoka mikono ya Firaun. Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam akasema, “Sisi tuna  haki zaidi juu ya Musa kuliko nyinyi” Akafunga na akaamrisha watu wafunge. ( Bukhaari)

Nini tutarajie? Kusamehewa Madhambi yetu (madogo madogo) ya mwaka mzima uliopita. ( Muslim)

Tumia fursa hii adhimu na adimu kujikurubisha kwa Allaah Subhaanahu Wata’ala kwa kufunga na kuomba Maghfira na pia kumfuata Mtume wetu na kipenzi chetu ambaye alijihimu na kujitahidi kufunga katika siku kuliko siku nyengine yoyote ya mwaka ( isipokuwa siku za Ramadhaan).

Please join the rest of Muslim Ummah by fasting these two important days in Islaam. All are welcome to join.

Tafadhali ukikufika ujumbe huu Mkumbushe Muislamu mwenzako.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.