
Leo
jioni timu ya Taifa ya Zanzibar – Zanzibar heroes itajitupa uwanjani kuvaana na
timu ya taifa ya Kenya – Harambee Stars katika mchezo wa nusu fainali kugombea
kombe la Cecafa katika uwanja wa Mandela mjini Kampala Uganda.
Zanzibar
Heroes iliweza kufikia nusu fainali baada ya kuitoa timu ya taifa ya Burundi
kwa mikwaju ya penelti baada ya mcezo kumalizika bila ya kufungana.
Kibarua
cha leo ni kigumu sana ukizingatia timu ya Taifa ya Kenya ni mojawapo katika
timu nzuri zilizoonesha kandanda la kuvutia na pia Kocha wa Kenya ameongeza
timu yake baada ya kuwaita wachezaji wawili aliowaacha nyumbani kutokana na
utovu wa nidhamu.
Ingawa
Zanzibar Heroes haina rekodi nzuri dhidi ya Harambee stars kwani katika mara 11
zilizowahi kukutana katika mashindano haya Kenya imeshinda mara saba, kutoka
sare mara tatu na imefungwa mara moja tu. Hata hivyo kinachoshindaniwa hapa si
rekodi bali uimara wa timu tuliyo nayo
Heroes
hata hivyo wapo katika hali nzuri kisaikolojia kwa kuweza kuziondoa timu kubwa
zenye majina hivyo Harambee Stars itajikuta ina wakati mgumu jioni ya leo kwani
ari ya ushindi kwa vijana wetu imezidi kuongezeka licha ya timu hii kupata
maandalizi dhaifu na hafifu ambapo walikosa mechi za maana za kujipima nguvu
kabla ya mashindano haya.
Hata
hivyo soka walilolionesha, kujiamini kwa wachezaji wetu huku kila mmoja akijua
nini wajibu wake akiwa uwanjani, kusikiliza ushauri wa kocha Salum Bausi, ni
vitu muhimu vilivyoisaidia timu yetu kufanya vizuri na kufika nusu fainali.
Nahodha
wa Zanzibar Heroes Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema ‘ Haoni timu nyengine
itakayowasumbua baada ya kuiondoa Burundi kwenye robo fainali’.
Kiungo Suleiman Kassim 'Selembe' ndiye anaonekana kuwatia khofu wakenya kwani ndiyo injini ya timu ya Zanzibar hivyo wanatarajia kumkaba ilivyo.
Katika
michezo ya nusu fainali mwaka huu mashindano ya Cecafa yamebakiwa na timu nne
ambazo ni waasisi wa mashindano haya mwaka 1947 nao ni Kenya, Tanganyika,
Uganda na Zanzibar.
Blog
ya ZanziNews inaitakia kila la heri Zanzibar heroes leo hii na ituletee raha
kwa kuwaondoa wakenya na kusubiri mchezo wa fainali ambao tuna imani ya
kulirudisha kombe la Cecafa kama tulivyofanya mwaka 1995.
Come
on Heroes
Good luck heroes
ReplyDeleteAfadhali 'Cholo' amerudi asidie kuimarisha ukuta kule nyuma!
ReplyDelete