Habari za Punde

Wadau waomba kuanzishwa Mahakama ya kusimamia haki za Wanyama


 
 


 KATIBU wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Asma Jidawi katikati, akitoa maelezo juu ya njia ya kuchangia mada baada ya kuwasilishwa kwa marekebisho ya sheria namba 11 ya mwaka 1999 ya kuwalinda wanyama, mbele ya wadau wa kutetea haki za wanyama kwenye mkutano wa siku moja uliofanyika ukumbi wa Magofu Chake chake Pemba jana kulia ni mwanasheria Khamis Mwita
 
Na Haji Nassor, Pemba
 
WADAU wa kusimamia haki za wanyama,wamependekeza kuanzishwa kwa Mahakama maalum itakayosikiliza kesi za ukatili wa wanyama, ili kupunguza ukatili huo uliokithiri kwa wafugaji na watumiaji wengine.
Walisema katika siku za hivi karibuni kumejitokeza kwa kiwnago kikubwa ukatili dhidi ya wanyama na ndege, bila ya watendaji wa ukatili huo kujali wakijua kuwa hakuna adhabu itayowakumba
Wadau hao walieleza hayo jana huko ukumbi wa Magofu Chake chake wakati walipokuwa wakichangia marekebisho ya sheria namba 11 ya mwaka 1999 ya kuwalinda wanyama ilipowasilishwa na wanasheria kutoka Tume ya marekebisho ya sheria kupitia Wizara ya Katiba na Sheria.

Walieleza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikichangiwa na kutokuwepo kwa Mahakama maalum za kushughulikia kesi za ukatili na udahililishaji wa wanyama, hivyo kama Wizara husika itanzisha mahakama hiyo, vitendo hivyo vinaweza kupungua kwa kasi.
Mgeni Said Mgeni kutoka kituo cha Polisi Chake chake, alisema pamoja kwamba kwa baadhi ya wakati kesi mbali mbali hucheleweshwa kuanzia Jeshi la Polisi , Mahakamani na jamii yenyewe, lakini kuwepo kwa Mahakama ya wanyama itasaidia.
Alifafanua kuwa wamiliki wa wanyama kama vile Punda na Ng’ombe wamekuwa mstari wa mbele kutumikisha bila ya kiasi kwa kupakiwa mizigo mizito bila ya kupewa muda maalum wa kupunzika.
‘’Wenye gari za Ng’ombe na Punda wamekuwa wakiwapakia wanyama wao mizigo mingi na bakora juu, na anapita mbele ya vyombo vya sheria, lakini sheria dhaifu na kutokuwepo kwa mahakama ya wanyama kumechangia kuendelea’’.alifafanua.
Nae sheha wa Shehia ya Ndagoni Massoud Ali Mohamed alisema uhaba wa madaktari wa wanyama kwa baadhi ya wakati, huchangia kuingizwa kwa wanyama kutoka nje ya Kisiwa cha Pemba bila ya kuchungzwa.
Alieleza kuwa wakati mwengine wanyama hao wamkuwa na maradhi lakini hata wanapowakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria, hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.
Mapema wakiwasilisha sheria hiyo na historia yake, mwanasheria kutoka Tume ya Marekebisho ya sheria Ali Mohamed, alisema sheria hiyo baadhi ya vifungu haviendani na wakati uliopo ikiwa ni pamoja adhabu ndogo kwa mkatili wa wanyama.
Nae mwanasheria Khamis Mwita wakati akiwasilisha maoni ya sheria hiyo namba 11 ya mwaka 1999 kutoka kwa wanasheria alisema, wamebaini kuna vipengele kadhaa ambavyo havikidhi haja kwa wakati huu
‘’Kifungu cha 36 kilikuwa kinamuelekeza sheha na afisa mifugo kumshika mtu aliefanya ukatili dhidi ya wanyama, lakini sisi tukapendelea sheha asiwe mkamataji bali atoe taarifa kwa vyombo vya sheria’’,alieleza Mwita.

Tume hiyo ya marakebisho ya sheri ipo Kisiwani Pemba kukutana na wadu mbali mbali ikiwa ni pamoja wafugaji, wataalamu wa mifugo, maofisa Wilaya wa mifugo ili kukusanya maoni ya kuifanyia marekebisho ya sheria hiyi namba 11 ya mwaka 1999 ya kuwalinda wanyama.

2 comments:

  1. Mambo ya ajabu haya...!
    Ikiwa mahakama za kusimamia haki za w'damu zinatushinda itakua za wanyama?

    Mfano mzuri ni lile jengo la mahakama kuu pale Viga utadhani lililohamwa!..kitu cha msingi hapa ni kupitisha mswaada wa kulinda wanyama utakaosimamiwa kisheria na kitengo ndani ya mahakama zetu!

    ReplyDelete
  2. wallahi kichekesho nasema kichekesho kwa nn ? kwa sababau zanzibar hakuna justice kabisa haheshimiwi bibadamu atatendewa haki mnyama .na kiilivyo mnayama pia anatakiwa apewe haki kama kiumbe chengine asiteswe na apate mahitaji yote muhmu kwa mmiliki wake au kwa serikali . lkn kwetu hatuna hayo wanyam wanazurura ovyo na wamechoka wanajitafutia rizki wenyewe majaani huko kwa mahakama ya wanyama zanzibar hiyo itakua ni ndoto mnajidanganya wala msizungumze tena mnatia aibu bora mnyamaze tu. msizungumze vitu ambavyo mnajua kama havitakuja ku work zanzibar.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.