Habari za Punde

Wawili wafa Musoma



Na Pascal Michael, Musoma
WATU wawili wamekufa katika matukio mawili tafauti akiwemo mtu  mmoja  anayefahamika  kwa jina la Kashimiri   Suleman Ndobo  (40) mkazi wa Buhare manispaa ya Musoma  alikutwa  akiwa amekufa na mwili wake kutupwa katika gofu la nyumba.

 Hayo yamesemwa  jana na Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Kamishina msaidizi Absalom Mwakyoma   wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari.

Mwakyoma alisema  marehemu  wakati wa uhai wake aliwahi kuwa Afisa Utamaduni  kabla ya kuacha kazi  kutokana na maradhi  ya akili yaliyosababishwa na  kuchanganyikiwa.


Polisi wanaendelea na uchunguzi kujua chanzo cha kifo chake.

Katika tukio la pili mtu mmoja  asiyejulikana   jina  amekutwa  amefariki dunia  katika eneo la Makoko  manispaa ya Musoma.

Mwakyoma alisema mwili wa marehemu  anaekadiriwa  kuwa na umri kati ya miaka 24 -27 ulikutwa umetupwa kando ya Ziwa   Victoria.

Alisema hadi sasa hakuna  mtu aliyeutambua  mwili huo na maiti imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia  maiti katika hospitali ya mkoa wa Mara kwa ajili ya uchunguzi wa kidaktari.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.