Na Mwantanga Ame
MWENYEKITI wa taasisi ya utafiti na sera za kijamii (ZIRPP) Mohammed Yussuf
Mshamba, amesema wananchi hawapaswi kuwa na wasiwasi juu ya nafasi ya Masheha
katika kuunda mabaraza ya bunge la katiba ya Jamhuri ya Muungano wakati
utakapowadia.
Mshamba alitoa tamko hilo baada ya washiriki kuonesha mashaka
kwamba iwapo Masheha watatumika kwa kazi hiyo mabaraza hayo huenda yakawa na
sura ya chama kimoja.
Mwenyekiti huyo aliyasema hayo baada ya baadhi ya wadau wa taasisi hiyo
waliojitokeza kutoa maoni yao juu mtazamo wao
katika katiba mpya kikao ambacho kilifanyika Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Aliwaambia washiriki wa mkutano huo kwamba masheha watakuwa na jukumu dogo sana katika utekelezaji wa
kazi hizo.
Hata hivyo Mwenyekiti huyo alijikuta katika wakati mgumu kujibu maswali juu
ya uamuzi wa tume hiyo kuyafanya siri
maoni juu ya Katiba mpya yanayotolewa na viongozi.
Wadau wa taasisi hiyo waliotaka kufahamu sababu za tume kufanya siri maoni
ya viongozi wastaafu na wajumbe wa tume kuvuruga mtazamo wa wananchi kwa
kuwaingilia wanapotoa maoni.
“Jambo hilo ni gumu kwangu, siwezi kulitolea maelezo,” alisema na kuongeza “mimi nazungumza hapa kama mtendaji wa
ZIRPP.”
Abbas Juma Mhunzi, Mwakilishi wa zamani wa jimbo la Chambani alisema utendaji wa tume unatia shaka hasa
pale viongozi wake wanawapoingilia kwa kutokubaliana moja kwa moja na baadhi ya
maoni yanayotolewa na wachangiaji mbele ya tume hiyo.
Mapema washiriki katika mkutano huo walilalamika kwamba katika mikutano
kadhaa, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba hakuwatendea haki wananchi kwa kuwaingilia
watoa maoni akionyesha wazi kutokubaliana na mtazamo wao.
Maeneo yaliyotajwa kutokea kwa hali hiyo ni pamoja na Singida ambako Jaji
Warioba alibishana na mtoa maoni kwa
kumwambia, mfumo wa serikali tatu anaotaka una gharama kubwa, hasa kwa
kuzingatia tatizo la gharama za uendeshaji zinazoukabili hata huu wa serikali
mbili.
Akimtetea Muhammed alisema kimsingi moja ya kazi za tume ni kuwaongoza wananchi ili waweze kutoa maoni
kwa usahihi na kuyaheshimu mawazo yao
na kwamba anaamini hivyo ndivyo anavyofanya Jaji Warioba.
Mimi naamini wasiwasi wa wananchi kwa masheha sio kua inaleta sura ya chama kimoja bali unatokana na iwango kidogo cha elimu walichonacho masheha.
ReplyDeleteZ'bar imebaki sehemu pekee duniani ambapo elimu haipewi kipao mbele,...sasa wacha sisi tupeleke masheha, wenzetu wapeleke watu waliosoma baadae tuje tuseme tunaonewa.
Waswahili husema "wajinga ndio waliwao"