Habari za Punde

Rais Kikwete atembelea majeruhi walioumia kutokana na jengo lililoporomoka

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole Bw. Selemani Saidi, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25 Kushoto mwenye suti nyeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Raymond Mushi Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya Moi.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam wakimpa pole kijana Mohamed Ally Dhamji ambaye ni miongoni mwa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole kijana Baqir Dhamji, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25. Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya MOI.

PICHA NA IKULU
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo Machi 31, 2013 ametembelea Hospital ya Taifa ya Muhimbili  kuwapa pole majeruhi walioumia katika ghorofa lililoporomoka juzi Ijumaa Machi 26, 2013 katika Mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 20.
Rais Kikwete, akiwa ameongozana na mke wake, Mama Salma Kikwete, pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Mhe. Hawa Ghasia, aliwatembelea na kuwapa pole majeruhi Mohamed Ally Dhamji, Baqir Virani, Selemani Saidi na Yusuf Abdallah  waliolazwa Taasisi ya Mifupa (MOI).
Majeruhi hao, ambao kwa mujibu wa Daktari C.N. Mcharo wanaendelea vyema na matibabu na hali zao ni za kuridhisha, ni wanne ni kati ya sita waliolazwa katika taasisi hiyo, ambapo wawili wamekwisharuhusiwa.
 "Poleni sana kwa maumivu mliyoyapata na nawatakia mpate nafuu ya haraka", Rais Kikwete aliwaeleza majeruhi hao, walionusurika baada ya kuangukiwa na jengo hilo la ghorofa 16 lililoporomoka ghafla likiwa katika ujenzi.
 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
31  Machi, 2013
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.