Habari za Punde

Hadithi ya Leo (3)


Amesema Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi wasallam

: الصِّيَامُ وَالْقُرْآنُ يَشْفَعَانِ لِلْعَبْدِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، يَقُولُ الصِّيَامُ: أَيْ رَبِّ مَنَعْتُهُ الطَّعَامَ وَالشَّهَوَاتِ بِالنَّهَارِ، فَشَفِّعْنِي فِيهِ. وَيَقُولُ الْقُرْآنُ: مَنَعْتُهُ النَّوْمَ بِاللَّيْلِ فَشَفِّعْنِي فِيهِ. قَالَ: فَيُشَفَّعَانِ».

Funga na Qur’aan zitamwombea mja siku ya kiama. Funga itasema (siku hiyo),  Ewe mola nilimzuia kula na matamanio muda wote wa mchana ( wa funga) hivyo Ninamuombea shufaa yako. Na Qur’aan (siku hiyo) itasema; nilimkosesha usingizi wakati wa usiku (kwa sababu ya kunisoma wakati wa ibada) hivyo ninamuombea shufaa yako. Na maombi ya shufaa yatatakabaliwa .

Imepokewa na Ahmad

Ewe Mola tujaalie kuifunga funga uliyoitambulisha kwetu kwamba ni yako ili iwe ndio mkombozi wetu wa kutuokoa na adhabu zako siku ya kiama.

Ewe Mola tujaalie kuisoma Qur’aan tutakayojaaliwa kuisoma katika mwezi huu adhimu iwe ndio mkombozi wetu wa kutuokoa na adhabu zako siku ya kiama.

Aamiyn Aamiyn

1 comment:

  1. naam ni kweli lakini sio kwa wale wanaofuturu kwa riziki zilizopatikana kwa fedha za haramu , na
    wengi ni namna hio , huchukua pesa za rushwa , au wakipanga bajeti za kununua vitu vya serikali au mashirika , basi hutia kamisheni zao humo , hizo zote ni pesa za haramu ,hazifai kununua chakula na kufuturia kwenye funga

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.