Mtume
Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam amesema:
رحم الله رجلاً قام من الليل فصلي ،ثم أيقظ امرأته
فصلت،فإن أبت نضح في وجهها الماء،ورحم الله امرأة قامت من الليل فصلت ثم أيقظت
زوجها فصلي ،فإن أبي نضحت في وجهه الماء " (رواه النسائي)
Allaah humrehemu
mwanamme anayeamka usiku na kusali
(Tahajjud) kisha akamuamsha mkewe naye akasali, na kama akikataa
humrushia (humnyunyizia) maji kwenye uso
wake ( ili aamke). Na Allaah humrehemu mwanamke anayeamka usiku na kusali
(Tahajjud) na kisha akamuamsha mumewe naye akasali na kama akikataa humrushia (humnyunyizia)
maji kwenye uso wake (ili aamke)
Imepokewa
na Annasaaiy
Hadithi
nyengine inayotuhimiza kujenga ushirikiano mkubwa kati ya mume na mke katika
kufanya ibada hasa za usiku mkubwa.
Mume
na mke wanapaswa kusaidiana katika kumtii Allaah Subhaanahu Wata’ala.
Ni
fursa nzuri kulitumia hili kumi la mwisho ambapo tuoeneshe njia na mfano wa
kuamshana na kuzitekeleza hizi ibada za usiku kwa ajili ya kupata radhi zake
Allaah Subhaanahu Wata’ala na kwa kuweza kulipwa malipo yasiyokuwa na hesabu
ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhaan, ndani ya siku kumi bora za mwisho wa
mfungo wa Ramadhaan.
No comments:
Post a Comment