Habari za Punde

Latif Primary School yatangaza nafasi za kazi za Walimu


NAFASI ZA KAZI
Latif Primary School ni skuli mpya ya kisasa inayotarajiwa kuanza kwa muhula wa kwanza wa  masomo mwaka 2014 inatangaza nafasi za ajira kwa ngazi zifuatazo.
1 Mwalimu Mkuu
Sifa za mwombaji
·       Awe angalau na Diploma ya Ualimu.
·       Awe si chini ya umri wa miaka 35
·       Awe na uzoefu  wa angalau miaka miwili katika nafasi ya  Uwalimu mkuu, mkuu wa idara au nafasi yoyote ya uongozi katika elimu.
·       Awe na uzoefu  wa kusomesha usiopungua miaka 5
·       Mwombaji mwenye diploma ya uongozi (management) atakuwa na kigezo cha nyongeza (added advantage)
·       Awe ni mwenye tabia njema na mwenye kuheshimika
·       Awe na uwezo wa kutumia computer hasa program za Microsoft Office
·       Awe na uwezo wa kuzungumza,kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha

2 Walimu wa kawaida (darasa la kwanza mpaka la tatu)
Sifa za mwombaji
·       Awe angalau na Diploma ya ualimu msingi kati ya masomo ya Kiswahili English, Hesabati, Kiarabu, Dini, au Mazingira.
·       Awe si chini ya umri wa miaka 25
·       Awe na uzoefu  wa kusomesha usiopungua miaka miwili
·       Awe na uwezo wa kuzungumza,kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha
·       Uwezo wa kutumia computer utapewa kipaumbele


3 Msimamizi wa ofisi
Sifa za mwombaji
·       Awe angalau na Diploma ya uhasibu
·       Awe si chini ya umri wa miaka 25
·       Awe na uzoefu  wa kazi usiopungua miaka miwili
·       Awe na uwezo wa kuzungumza,kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha
·       Uwezo wa kutumia computer ni lazima


Jinsi ya kutuma maombi
·       Barua za maombi ziambatanishwe na maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) pamoja na picha mbili za Passport size za hivi karibuni moja iandikwe jina nyuma
·       Kwa urahisi wa mawasiliano, waombaji waonyeshe anwani na namba za simu za kuaminika, na barua pepe kama anayo
·       Maombi yote yaambatane na nakala za vyeti vya kidato cha nne na  vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
·       Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 9 Disemba 2013 saa 11 jioni
·       Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na mwombaji anaweza kuwasilisha maombi yake kwa mkono kwa kufika jengo la skuli liliopo Malindi nyuma ya msikiti wa Ijumaa wa malindi  karibu na Pyramid Hotel.  
·       Pia yanaweza kutumwa  kwa njia ya posta au barua pepe kupitia anuani ifuatayo.
Mwenyekiti wa kamati
Latif Primary School
SLP 860
Zanzibar
Barua pepe almdrasatullatif@gmail.com
Nambari za simu : 0777 416 723 au 0772 000 550













NAFASI ZA MASOMO
Pia skuli hii inapenda kuwatangazia wananchi kuwa inaanza kupokea maombi ya wanafunzi wa darasa la kwanza mpaka la tatu kwa masomo ya msingi kwa muhula mpya wa mwaka 2014.
Latif Primary School ni skuli mpya na ya kisasa iliyopo Malindi, Zanzibar.  Ni skuli Inayozingatia maadili ya Kiislamu na pia yenye kutoa elimu ya kisasa ikiwemo masomo ya computer
Fomu za uandikishaji zinapatikana katika jengo la skuli.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana nasi kupitia simu nambari 0777 416723 au   0772 000 550. Pia kwa kupitia barua pepe: almdrasatullatif@gmail.com
Pia unaweza kufika katika jengo la skuli liliopo Malindi nyuma ya msikiti wa Ijumaa wa Malindi karibu na Pyramid Hotel 

3 comments:

  1. Ni bahati hiyo kwa ndugu zetu waalimu hasa wale ambao wamekua wakisubiri ajira kwa mda mrefu bila mafanikio.

    Hata hivyo sidhani kama sifa zilizotajwa zinaweza kupatikana miongoni mwa walimu wa kizanzibari. kutokana na sababbu zifuatazo:

    1) Hapa kwetu Ualimu mkuu ni cheo ambacho mwalimu hukisubiri kwa mda mrefu na anapobahatika kukipata hawezi kuacha kazi mwenyewe labda afukuzwe.

    2) Walimu wenye Diploma za uongozi, umri na uzoefu uliotajwa wengi wapo SMZ sidhani kama kuna mwl. mwenye ujasiri wa kuacha kazi na kwenda LATIF kwa utamaduni wetu hapa!

    Wataishia tu kuwapata walimu wastaafu (washao choka) au wale ambao hawajaajiriwa!

    ReplyDelete
  2. Hapa ninapoishi ni kawaida kutajwa mshahara katika tangazo la kazi.
    Sasa nauliza mishahara ni kiasi gani kwa kulingana na nafasi hizo za kazi ?

    ReplyDelete
  3. Ni kweli kama ulivosema Anonymous wa kwanza kwamba ni ngumu kupata wenye viwango hivo ambao watakuwa tayari kujiunga na Latif.

    Anonymous wa pili, kama unataka kujua zaidi kuhusu kazi au mishahara si uwapigie simu tu upate taarifa zaidi? Si kila kitu kinaendana na ulivyozowea wewe

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.